logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Mlima wote, baba tosha" Ben Githae afanya upya wimbo wake 'Tano tena' kupigia debe Raila Odinga

Githae amesema amebadilisha wimbo huo ambao alibuni  takriban miaka mitano iliyopita kupigia debe rais Uhuru Kenyatta ili sasa uweze kutumika katika kampeni za Raila Odinga.

image
na Radio Jambo

Habari16 November 2021 - 10:32

Muhtasari


•Githae amesema amebadilisha wimbo huo ambao alibuni  takriban miaka mitano iliyopita kupigia debe rais Uhuru Kenyatta ili sasa uweze kutumika katika kampeni za Raila Odinga.

•Amewasihi wakazi wa Pwani wampigie kura kinara wa ODM mwaka ujao huku akidai eneo la Mt Kenya tayari limeamua kuunga mkono azma yake ya kuwania urais kwa mara ya tano.

Mwanamuziki mashuhuri wa nyimbo za injili na kisiasa Ben Githae ameufanya upya wimbo wake 'Tano tena' kuugeuza kuwa wa kupigia debe kinara wa ODM Raila Odinga.

Alipokuwa anatoa hotuba yake katika mkutano wa siasa uliofanyika Kwale asubuhi ya Jumanne, Githae alisema ameamua kubadilisha maneno ya wimbo wake kuona kwamba eneo la mlima Kenya linamuunga mkono kinara wa ODM.

Githae amesema amebadilisha wimbo huo ambao alibuni  takriban miaka mitano iliyopita kupigia debe rais Uhuru Kenyatta ili sasa uweze kutumika katika kampeni za Raila Odinga.

"Mimi ni Ben Githae yule alisema 'Tano tena' na 'Wembe ni ule ule' . Saa hii tumegeuza huo wimbo tunasema 'Ndani ndani ndaniii to the state house, mlima wote baba tosha'" Githae alisema.

Mwanamuziki huyo amewasihi wakazi wa Pwani wampigie kura kinara wa ODM mwaka ujao huku akidai eneo la Mt Kenya tayari limeamua kuunga mkono azma yake ya kuwania urais kwa mara ya tano.

Mwaka wa 2017 wimbo 'Tano tena' ulitumika sana kupigia chama cha Jubilee kampeni. 

Baada ya mahakama kutupilia mbali matokeo ya urais katikachaguzi hizo Githae alitoa wimbo 'Wembe ni ule ule' ambao ulitumika katika kampeni za marudio ya uchaguzi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved