logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Amepitia mengi-Aliyekuwa Meneja wa Tanasha Donna afichua aliyoyapitia Tanasha baada ya kuachana na Diamond

Aliongeza kuwa Tanasha amepitia mengi, na kuwa hawezi andika kitabu bila kumtaja Castro.

image
na Radio Jambo

Burudani21 November 2021 - 20:00

Muhtasari


  • Aliyekuwa Meneja wa Tanasha  Donna afichua aliyoyapitia Tanasha baada ya kuachana na Diamond

African Castro, aliyekuwa meneja wa Tanasha Donna alisema kuwa mama huyo wa mtoto mmoja alipaswa kutafuta usaidizi wa kitaalamu baada ya kuachana na Diamond.

Akizungumza wakati wa mahojiano na Presenter Ali, Castro alisema kutengana huko kulifanya Tanasha kukosa mwelekeo.

"Drama ya  uhusiano uliathiri kasi tuliyokuwa nayo. Ukweli ni kwamba Tanasha aliumia baada ya kuachana na Diamond na hakupumzika kutafuta msaada kutoka kwa mtaalamu

Hapo ndipo niliponawa mikono yangu na kumuacha kwa meneja wake mwingine. Nilikutana na Tanasha alipokuwa mwanamitindo," Alio ngea Castro.

Aliongeza kuwa Tanasha amepitia mengi, na kuwa hawezi andika kitabu bila kumtaja Castro.

"Alifanya Tangazo na Safaricom na ndipo alipojulikana, baada ya hapo akaenda NRG,Kuna mengi ninaweza kusema juu yake na kuna mengi anaweza kusema kunihusu lakini tuliamua kutoyazungumza

Amepitia mengi. Unachokiona sasa ni athari yangu. Hawezi kuandika kitabu bila kunitaja."

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved