logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Je Diamond na Eric Omondi ndio watu mashuhuri zaidi Afrika Mashariki kama anavyodai Eric?

Aidha aliongeza kuwa yeye ndiye mtu mashuhuri anayezungumziwa zaidi na mwimbaji wa Tanzania Diamond.

image
na Radio Jambo

Habari22 November 2021 - 08:59

Muhtasari


  • Je Diamond na Eric Omondi ndio watu mashuhuri zaidi Afrika Mashariki kama anavyodai Eric?

Mchekeshaji asiyepunguwa na drama au vichekesho Eric Omondi, amejitangaza kuwa mcheshi maarufu zaidi kufikia sasa.

Katika mahojiano ya hivi majuzi na 10/10, Eric aliwaambia watu wanaomtaja kama mtafutaji kiki kwamba ni sehemu ya tasnia ya burudani na kwamba haipaswi kupuuzwa na ubunifu wowote.

"Nataka kufichua na kuwafahamisha wanaonihukumu na kuwafahamisha kuwa tasnia ya burudani ni Kiki- ni sehemu ya burudani,

Mimi sitafuti kiki. Kazi ya mchekeshaji ni kusukuma bahasha, kuvuka mipaka. Tunaruhusiwa kwa vile sisi ni kioo cha jamii," Eric Aliongea.

Eric aliongeza zaidi kwamba burudani ni kama bahari;

"Ni pana na ya kina na inachukua kila namna. Kile watu wengi hurejelea kuwa mshikamano ni burudani katika hali yake safi. Ninacheka sana ninapoendelea kusikia watu wakipiga simu. na kudai kwamba napenda kutafuta kiki."

Aidha aliongeza kuwa yeye ndiye mtu mashuhuri anayezungumziwa zaidi na mwimbaji wa Tanzania Diamond.

“Nataka kuitaarifu tasnia ya burudani kuwa wasanii wanaozungumziwa zaidi Afrika Mashariki ni Diamond Platnumz na Eric Omondi,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved