- Mwanamke asimulia masiabu ya ndoa yake, yaliyosababishwa na wakwe wake
Ndoa ukiwa nje huonekana kuwa kitu kizuri sana na hakuna mabaya huweza kutabiri au kujua baadhi ya changamoto ambazo zinaweza kuleta msukosuko katika uhusiano kati ya mume na mke .
Wakati watu wanapofanya mipango ya kufunga pingu za maisha ,wengi hujua kwamba basi wamefika mwisho kuhusu kuwahi kumtafuta mtu mwingine wa kuwahi kuishi naye maisha yao yote
Wengi wakati huo wa mwanzo mwanzo huwa hawafikirii kwamba wakati mwingine kuna sababu au watu wengine ambao huweza kuwa na ushawishi mkubwa wa kutengeza ama kuvunja ndoa yao .
Kuna wale wamepatana na wakwe ambao wanawapenda ilhali kuna baadhi ambao hawawezi kusikizana na wakwe wao kwa njia moja au nyingine.
Huku nikiwa kwenye ziara yangu nilipatana na mwandada anayeefahamika kama Benedicta, ambaye alinisimulia masiabu ya ndoa yake tangu alipofunga ndoa na mume wake mpendwa.
Kulingana naye wamekuwa kwa ndoa kwa miaka 8 lakini, sio ndoa ambayo alitamani alipokuwa msichana.
Benedicta ambaye ana watoto 2 anasema kwamba alaichana kusikizana na wakwe wake punde tu alipoingia katik afamilia yao.
"Baada ya harusi yetu mama mkwe alinitusi sana na nikavumilia,kwani mume wangu anamsikiza maama yake sana yaani yuseme ni 'mamas boy'
Tumeng'ang'ana miaka hiyo yote,lakini baada ya kuja kuishi Nairobu na mume wangu, wakwe wangu walimtafutia mke mwingine ambaye kwa sasa anaishi kwa nyumba yetu mashambani
Sikuona kuwa mama kwe anaweza kuwa na usemi kuhusu ndoa yetu nilipomuaona kwa mara ya kwanza, aliniambia ni siwahi rudi kwake, na baada ya kumwambia mume wangu anapumbazwa na mama yake na kumuunga mkono
Sijui maisha yangu yanaenda vipi, kwani niko kwenye dilema, kile naweza sema ni kuwa ndoa sio safari rahisi kwa maana utapatana na changamoto nyingi kuliko mafanikio ukiwa na wakwe ambao hawakupendi kamwe," Alizungumza.
Lakini swali kuu ni je nani wa kulaumiwa katika ndoa hii?