logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DJ Mo awashauri mashabiki jinsi ya kuwatunza wanawake wao

Akaendelea na kuwashauri wanaume wote pale nje kuwatunza vyema wapenzi wao

image
na Radio Jambo

Burudani24 November 2021 - 13:39

Muhtasari


  • DJ Mo awashauri mashabiki jinsi ya kuwatunza wanawake wao

DJ Mo ni mmoja wa watu mashuhuri wachache wa Kenya ambao haogopi kupongeza, kutoa zawadi na kusimama karibu na mke wake mpendwa.

Atamsifu mke wake Size 8 hadharani, amshike mkono wakati wa nyakati mbaya na kila mara atamwaga zawadi na kuwaonyesha wale wanaomtazama au uhusiano wao jinsi ya kumtunza mwanamke kama malkia.

Katika chapisho lake la hivi majuzi, baba huyo wa watoto wawili alichapisha picha ya mkewe na akashindwa kujizuia kughairi uzuri na utukufu wake.

Akaendelea na kuwashauri wanaume wote pale nje kuwatunza vyema wapenzi wao kwa sababu inazungumza mengi kuhusu wewe ni mwanaume.

"Jinsi unavyomtunza mwanamke wako, huonyesha sana wewe ni nani kama mwanaume," Aliandika DJ Mo.

Tumewaona wanandoa hao wawili wakipitia changamoto tofauti, huku wakiwaonyesha mashabiki wao kwamba licha ya hayo yote mapenzi yao yanazidi kunoga.

Pia ndoa yao ni ya kupigiwa mfano na wengi.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved