Natamani nipate mapacha,'Ujumbe wa Hamisa Mobetto ulio zua mdahalo mitandaoni

Muhtasari
  • Wengine wanaamini kuwa kuna kitu kilitokea kati yao walipokuwa Dubai, na kumfanya akubali kuwa anatamani mtoto
Hamisa 2
Hamisa 2

Hamisa Mobetto kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amewaacha  mashabiki wake na gumzo baada ya kusema kwamba anatamani kupata mapacha.

Kauli yake iliyonukuliwa ilizua taharuki kwa mashabiki na wafuasi wake. Kwa sababu alikutana na rapa wa Marekani Rick Ross huko Dubai na wawili hao wakawa marafiki katika klabu ambayo Rick Ross alikuwa akitumbuiza.

Wengine wanaamini kuwa kuna kitu kilitokea kati yao walipokuwa Dubai, na kumfanya akubali kuwa anatamani mtoto.

Haijafahamika iwapo wawili hao walienda vyumba tofauti baada ya kuondoka klabu pamoja usiku huo, lakini unadhani Hamisa ni mjamzito?

Akiwahotubia wanahabari wa Tanzania Hamisa aliweka wazi kwamba msanii Rick anataka kuwekeza katika Tanzania na wala wawili hao sio wapenzi.

"Natamani nipate mapacha alafu niwaite liwalo na liwe . πŸ’£," Aliandika Hamisa

Hizi hapa baadhi ya hisia za mashabiki;

expendable240: Vipi mama umenza kutapika????

makorokochokocho_2016: Alafu wafanane na dady yao nyie chapchap β€οΈπŸ™πŸΎ

lucky_okumu: πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ my ribs liwe should be a boy liwalo a gal

hildahaule86: Tumeshapata majina ya mapacha wakoπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚@sarahkamnde3783