Tuzo za Grammy: Uteuzi wa Drake waondolewa

Muhtasari
  • Kwa mujibu wa taarifa, uamuzi huo umetolewa kwa ombi la Drake na uongozi wake
  • Chanzo katika Recording Academy kimeiambia Newsbeat kwamba Academy ilichagua kuheshimu matakwa yake

Teuzi mbili za Drake za tuzo za Grammy kwa mwaka wa 2022 zimeondolewa kwenye tovuti rasmi.

Kwa mujibu wa taarifa, uamuzi huo umetolewa kwa ombi la Drake na uongozi wake.

Chanzo katika Recording Academy kimeiambia Newsbeat kwamba Academy ilichagua kuheshimu matakwa yake.

Sababu za hili kwa sasa hazijafahamika, na wawakilishi wa rapa huyo bado hawajajibu ombi la kutoa maoni.

Drake alikuwa mmoja wa walioteuliwa kuwania Albamu Bora ya Rap, ya Certified Lover Boy, na Wimbo Bora wa Rap, kwa Way 2 Sexy.

Kwenye tovuti rasmi ya Grammy inaeleza kuwa uteuzi huo umeondolewa, na hakuna mbadala, ikimaanisha kuwa upigaji kura kwa makundi hayo mawili utaendelea na wateule wanne pekee.

Drake amekuwa na uhusiano mgumu na Grammys siku za nyuma.

Mwaka jana aliomba ibaduilishwe na tuzo nyingine baada ya wasanii kadhaa wakiwemo The Weeknd kutozingatiwa.

"Nadhani tunapaswa kuacha kujiruhusu kushtushwa kila mwaka na kutengana kati ya muziki wenye athari na tuzo hizi," alisema wakati huo.

"Huu ni wakati mzuri kwa mtu kuanza kitu kipya ambacho tunaweza kujenga kwa wakati na kupitisha kwa vizazi vijavyo."

Mapema mwaka huu, wana Grammy walitupilia mbali kamati zao za upigaji kura ambazo hazikujulikana majina yao kufuatia madai ya wizi wa kura, upendeleo na ubaguzi wa rangi.

Chuo cha Kurekodi kilisema washiriki wake wa kupiga kura - ambao wanafikia maelfu - badala yake watachagua wateule na washindi wa mwaka ujao.