Wakenya watoa hisia tofauti baada ya Trio Mio kutangaza kuhudhuria hafla ya Raila Odinga Kasarani

Muhtasari
  • Wakenya watoa hisia tofauti baada ya Trio Mio kutangaza kuhudhuria hafla ya Raila Odinga Kasarani

Kupitia kwa video yenye urefu wa sekunde 33 ilyopakiwa mitandaoni na Raila, Trio aliwaambia mashabiki wake kuwa atahudhuria hafla ya Waziri  mkuu wa zamani  Raila Odinga ambapo anatarajiwa kutoa tangazo kuu.

Mwanamziki huyo wa kufoka aliwarai mashabiki wake kuhudhuria hafla hiyo ili kufahamu alichowabebea Raila Odinga.

Trio mwenye wimbo wa Sipangwinwgi aliwachekesha mashabiki katika video hiyo kwa kudai kuwa Raila ‘hapangwingwi’ kwani yeye ndiye wa kuwapanga watu.

“Ijumaa hii nitakuwa katika uwanja wa Kasarani kuhudhuria hafla ya Baba (Raila). Tujitokeze kwa ajili ya tangazo kubwa. Kama kawaida, huwa hapangwi, yeye ndiye hupanga,” Trio Mio alisema.

Video hiyo iliibua mdahalo mitandaoni huku wakeenya wakitoa hisa tofauti na hizi hapa baadhi ya hisia zao;

Shisia Bennie: If Trio Mio could have requested BABA @RailaOdinga to give him a chance to be at The Friday Event n Baba Turned him down koz of his age I swear Same Bitter People could have roasted BABA for Not giving a "young man " a chance.But it Must agend nyway. Mna Roho Chafu sana Huku.

Briph: Mnataka Trio Mio " without ID " to perform kwa clubs na events ziko fully sponsored na kampuni ya pombe but ku perform kwa campaign event ya Baba is where you all draw the line... Face with tears of joyFace with tears of joyFace with tears of joy mjidishi basi..

e.n.o.s.q.i: Trio mio sings about weed performs in clubs without ID but politics is where you guyz are seeing a mistake

Rachel Agunda:arachel·3hTrio Mio has been performing even in clubs but him being paid to perform at a political gathering is where you draw the line, now he has become too young to do it. Go get your money kid.