logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nishaazoea kuitwa sura mbaya,'Nyota Ndogo awakomesha wanaodai amezeeka

Pia amesema inaonekana kwamba yeye ni mrembo kuliko wapenzi wao wa miaka 20.

image
na Radio Jambo

Habari20 December 2021 - 09:31

Muhtasari


  • Inasemekana kuwa mtu Mashuhuri ni kama upanga  wenye makali kwenye pande zote mbili
  • Nyota Ndogo kupitia kwenye akaunti yake ya Instagram alifunguka jinsi amekuwa akipokea kejeli  kutoka kwa mashabiki kwa ajili ya sura yake

Inasemekana kuwa mtu Mashuhuri ni kama upanga  wenye makali kwenye pande zote mbili.

Hii ni kwa sababu mara moja umaarufu unakuja katika maisha ya mtu, mashabiki watawapenda na kukuchochea kwa sifa kila mahali unapoenda na kila kitu unachofanya.

Hata hivyo upendo huu kwa njia moja au nyingine unaweza kubadilika haraka kuhusiana na kile unachofanya au kile unachosema, na unaweza kwa bahati mbaya kuishia kupokea kejeli kutoka kwao

Nyota Ndogo kupitia kwenye akaunti yake ya Instagram alifunguka jinsi amekuwa akipokea kejeli  kutoka kwa mashabiki kwa ajili ya sura yake.

Kulingana na Nyota wengi wanaomkejeli ni wanaume, ambao wamekuwa wakifanya hayo baada ya kufikisha miaka 40 mwaka huu.

Aidha msanii huyo amesema kwamba amezoea kuitwa sura mbaya na kwamba wanapaswa kutafuta maneno mengine ya kumuita.

Pia amesema inaonekana kwamba yeye ni mrembo kuliko wapenzi wao wa miaka 20.

"Sasa kuitwa mazee na sura Mbaya nishazoea munaweza mukatafuta maneno makali mengine yakuniita na wengi wao uwa wanaume mybe I look much better at 40 kushinda your galfriend mwenye ako 25.hatukatai uzee uzee ni sunna ni hatizeeki kizembe hatujitupi wall yangu ikikusinya ni block," Amesema Nyota.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved