logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nawaonea wivu malaika juu wanakuona kila siku,' Willis Raburu amkumbuka marehemu bintiye kwa ujumbe wa kihisia

Raburu amekiri kwamba tangu Adana alipoaga huwa anapatwa na mchanganyiko wa hisia kila mwisho wa mwaka  kwani hajui ikiwa anafaa kusherehekea mwanzo wa mwaka mpya ama kuomboleza bintiye.

image
na Radio Jambo

Habari31 December 2021 - 09:35

Muhtasari


•Raburu amekiri kwamba tangu Adana alipoaga huwa anapatwa na mchanganyiko wa hisia kila mwisho wa mwaka  kwani hajui ikiwa anapaswa kusherehekea mwanzo wa mwaka mpya ama kuomboleza bintiye.

Mburudishaji na mtangazaji maarufu wa Citizen TV Willis Raburu amemkumbuka marehemu binti yake takriban miaka miwili baada yake kuaga.

Katika ukurasa wake wa Instagram Raburu amemnakilia bintiye Adana ujumbe maalum wa kihisia akiadhimisha siku ambayo marehemu alizaliwa.

Katika ujumbe wake Raburu amesema anatamani sana  angekuwa anasherehekea birthday ya pili ya bintiye pamoja naye huku akiongeza kwamba kwa kuwa sasa hayupo tena amebaki kuwaonea wivu malaika wa mbinguni ambao wanapata kumuona kila siku.

"Heri ya miaka 2 ya kuzaliwa Adana. Malaika wangu. Ninakufikiria kila wakati ninao. Ninakukumbuka na uso wako mzuri. Sitasahau kwani muda ule nilikuwa nawe katika chumba baridi na hata busu langu halingeweza kukurudisha hai! Nadhani hiyo inafanyika katika hadithi za hadithi tu. 😔💔 Nilipaswa kuwa nikisherehekea hatua zako muhimu lakini badala yake nimekaa hapa nikionea malaika wivu kwa sababu wanapata kuwa nawe kila siku." Raburu aliandika.

Amekiri kwamba tangu Adana alipoaga huwa anapatwa na mchanganyiko wa hisia kila mwisho wa mwaka  kwani hajui ikiwa anapaswa kusherehekea mwanzo wa mwaka mpya ama kuomboleza bintiye.

"Siku zote  kama hii ni siku ngumu kwa sababu sijui kusherehekea mwaka mpya au kuomboleza. Najua ungetaka tukusherehekee na ndio maana niko hapa. Piga kelele nyingi mbinguni leo wajulishe wazazi wako ni akina nani! 😢 Nakupenda. Mama na baba watakupenda milele na milele! 🙏🏾💔❤️😇" Aliandika Raburu.

Binti ya mtangazaji huyo alifariki wakati aliyekuwa mke wake Marya Prudence alikuwa anajifungua mnamo Desemba 31, 2019.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved