logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Wacha kutafuta kiki ni 2022,' Willy Paul amwambia Ringtone baada ya madai ameiba kibao chake

Pia alimhakikishia kwamba anampa heshima kwani ni yeye alimtangulia katika tasnia ya usanii.

image
na Radio Jambo

Habari04 January 2022 - 07:33

Muhtasari


  • Willy Paul amshauri Ringtone kuacha kutafuta kiki

Msanii Willy Pail almaarufu Pozze ameonekana kugadhabishwa na matamshi yake msanii wa nyimbo za injili Ringtone.

Hii ni baada ya Ringtone kudai kwamba kibao chake Willy Paul kinachofahamika kama 'Atoti Jaber' alikiiba kutoka kwake.

Kupitia kawenye ukurasa wake wa instagram Paul alimwambia msanii huyo kwamba kibao hicho hakijawahi kuwa cha inili na kwamba huu ni mwaka mpya anapaswa kuacha kutafuta kiki.

Pia alimhakikishia kwamba anampa heshima kwani ni yeye alimtangulia katika tasnia ya usanii.

"Wale mnaojua Ringtone mnajua yeye ni mtu wa aina gani.. Ndugu yangu tafadhali acha kuwaambia marafiki zako kuwa nilikuibia wimbo wa atotijaber. Haijawahi kuwa wimbo wa injili, inatosha na wacha ktafuta kiki kaka, Ni 2022, mwanzo mpya. Ninakupenda na kukuheshimu kama kaka mkubwa aliyekuja kwenye tasnia hii kabla yangu," Alisema Pozze.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved