logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Bill inapanda excess,'Sandra Dacha afichua Akuku Danger anaendelea vyema,licha ya bili ya hospitali kuongezeka

Dacha hata amefichua kwamba Akuku kwa mara ya kwanza aliomba chakula

image
na Radio Jambo

Burudani04 January 2022 - 19:26

Muhtasari


  • Dacha hata amefichua kwamba Akuku kwa mara ya kwanza aliomba chakula baada ya hali yake kuonekana kuwa nzuri

Mcheshi wa Kipindi cha Churchill Akuku Danger yuko hospotalini kwa siku ya saba hii leo  katika Hospitali ya Nairobi West chini ya Chumba cha Wagonjwa Mahututi.

Tofauti na hali yake ya awali ya afya, mcheshi huyo anapata nafuu taratibu kama ilivyofichuliwa na rafiki yake Sandra Dacha.

Kwa kweli, Dacha hata amefichua kwamba Akuku kwa mara ya kwanza aliomba chakula baada ya hali yake kuonekana kuwa nzuri.

"Akuku Danger hatimaye ameomba chakula, Haleluya. Njaa sio kitu kizuri." Dacha alifichua.

Hata hivyo, licha ya uboreshaji ulioshuhudiwa, Dacha ameambulia changamoto moja tu katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi.

Kulingana na Dacha, bili ya hospitali imekuwa ikiongezeka kwa kasi katika kipindi kifupi na ndani ya siku sita; bili ya matibabu sasa inafikia Ksh.1.5 milioni.

"Bill inapanda excess wuueh, imekuwa siku sita na tuko milioni 1.5." Dacha alisema.

Hata hivyo, hakupata wasiwasi mwingi kuhusu hilo lakini alifurahi tu kwamba Akuku alikuwa akipata nafuu.

Aidha, Dacha alitoa shukrani zake kwa mashabiki wote walioshiriki katika michango na maombi kwa ajili ya Akuku Danger.

Alipohitimisha, aliwaomba Wakenya kuendelea nao hadi tabu yao ikamilike.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved