logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Utaanguka! Bobi Wine amhutubia Museveni katika wimbo mpya

Amesema kwamba  alilazimika kufichua uhalifu uliofanywa chini ya utawala wa rais ndio sababu picha zilizotumika kwenye video zinatisha

image
na Radio Jambo

Habari05 January 2022 - 11:16

Muhtasari


•Amesema kwamba  alilazimika kufichua uhalifu uliofanywa chini ya utawala wa rais ndio sababu picha zilizotumika kwenye video zinatisha.

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda na mwanamuziki Bobi Wine ameachia wimbo mpya kwa jina Ogenda, neno la Kiganda linalomaanisha "Utaanguka".

Wimbo huo unamlenga Rais Yoweri Museveni moja kwa moja kwa sababu amekiuka ahadi yake kuleta demokrasia nchini, anasema.

Bobi Wine ameambia BBC  kwamba alilazimika kufichua uhalifu uliofanywa chini ya utawala wa rais ndio sababu picha zilizotumika kwenye video zinatisha.

"Utawala nchini Uganda umewekeza pesa nyingi kuficha ukatili huo," alisema.

Bobi Wine alisema vyombo vya habari nchini Uganda vimezimwa na njia pekee ya kufichua uozo huo ni kupitia muziki.

"Haki inaweza kupatikana pale tu tunapofichua uhalifu, ndiyo maana tunaendelea kuuibua, hiyo ndiyo njia pekee tunayoweza kupambana nayo," alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved