logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Tumekaribia kufika, endeleeni kuniombea" Akuku Danger azungumza kuhusu afya yake

Dacha amefichua kwamba mchekeshaji huyo anatarajiwa kuruhusiwa kutoka hospitali mnamo Jumamosi.

image
na Radio Jambo

Burudani14 January 2022 - 05:08

Muhtasari


•Akuku amesema anawathamini wote ambao wamekuwa wakimwombea, kumfariji na ambao wamechangia bili yake ya hospitali huku akiwahakikishia kwamba afya yake inaendelea kuimarika.

•Dacha amefichua kwamba mchekeshaji huyo anatarajiwa kuruhusiwa kutoka hospitali mnamo Jumamosi.

Akuku Danger

Mchekeshaji wa Churchill Show Mannerson Oduor Ochieng almaarufu kama Akuku Danger amezungumza na wanamitandao kwa mara ya kwanza tangu alipoanza kuugua mwezi uliopita.

Kupitia kanda ya video iliyochapishwa na mwandani wake Sandra Dacha (Silprosa) kwenye mtandao wa Instagram, Akuku Danger amewashukuru wote ambao wamekuwa wakisimama naye katika kipindi hiki kigumu maishani mwake.

Akuku amesema anawathamini wote ambao wamekuwa wakimwombea, kumfariji na ambao wamechangia bili yake ya hospitali huku akiwahakikishia kwamba afya yake inaendelea kuimarika.

"Shukran kila mtu kwa kuonyesha upendo, kwa usaidizi wenu na maombi. Kwa wale ambao wameonyesha upendo, kwa waliochangia bili ya hospitali na wanaoendelea kuchanga nawashukuru sana kutoka moyoni mwangu. Tunakaribia kufika pale , endeleeni kuniombea na nawathamini nyote" Akuku amesema.

Dacha amefichua kwamba mchekeshaji huyo anatarajiwa kuruhusiwa kutoka hospitali mnamo Jumamosi.

Amewasihi Wakenya kuendelea kuchangia bili ya hospitali ya Akuku ili kumwezesha kuachiliwa  kwenda nyumbani.

"Tafadhali tusaidieni kupeleka Akuku Danger nyumbani, tafadhali. Ataruhusiwa kwenda nyumbani kesho. Paybill 891300 ACC (Weka jina lako)" Dacha amesema kupitia ukurasa wake wa Instagram

Wanamitandao wameendelea kumtakia mchekeshaji huyo afueni ya haraka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved