logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Otile Brown atoa taarifa nzuri kuhusu afya yake baada ya upasuaji

Wiki iliyopita Brown alitoa taarifa ya kutia wasiwasi kuhusu afya yake.

image
na Radio Jambo

Burudani17 February 2022 - 08:22

Muhtasari


•Mwanamuziki huyo ametoa taarifa mpya kuhusu afya yake huku akifichua kuwa afya yake imeendelea kuimarika.

•Nabbi ambaye alitengana na Otile Brown wiki chache zilizopita amemtakia baraka na ulinzi wa Mola katika siku zote za maisha yake.

Mapema mwezi huu mwanamuziki mashuhuri Jacob Obunga almaarufu kama Otile Brown alifanyiwa upasuaji katika hospitali moja jijini Nairobi.

Brown alitangazia mashabiki wake kuhusu upasuaji huo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo alipakia video iliyoonyesha akiwa amelazwa kitandani cha hospitali na akaeleza kuwa shughuli hiyo iliendelea vizuri.

Siku chache baadae hata hivyo, Brown ambaye anashabikiwa sana hasa katika kanda ya Afrika Mashariki alitoa taarifa ya kutia wasiwasi kuhusu afya yake.

"Nina maumivu makali sana..ombeeni Obizee" Brown alitangaza kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Siku ya Jumatano mwanamuziki huyo alitoa taarifa mpya kuhusu afya yake huku akifichua kuwa afya yake imeendelea kuimarika.

Otile aliendelea kutangaza kuwa atakuwa anasafiri kuelekea Bahrain ambako atatumbuiza Jumatano wiki ijayo.

"Obizee anaendelea vyema.. Bahrain, naja wiki ijayo, Jumatano tarehe 23" Otile alitangaza.

Mamia ya mashabiki wameendelea kumtakia msanii huyo afueni ya haraka tangu alipotangaza kuhusu upasuaji.

Mpenzi wake wa zamani Nabayet almaarufu kama Nabbi ni mmoja wa waliomkumbuka katika kipindi hiki kigumu. 

Nabbi ambaye alitengana na Otile Brown wiki chache zilizopita amemtakia baraka na ulinzi wa Mola katika siku zote za maisha yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved