logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mungu wetu ni wa upendo-Rose Muhando amtakia Professor Jay afueni ya haraka

kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amemtakia Jay afueni ya haraka.

image
na Radio Jambo

Habari03 March 2022 - 09:32

Muhtasari


  • Nyota wa nyimbo za injili Rose Muhando, kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amemtakia Jay afueni ya haraka
Mwanamuziki Joseph Haule almaarufu kama Profesa Jay

Nyota wa muziki kutoka Tanzania Joseph Leonard Haule almaarufu kama Professor Jay anaendelea kupokea matibabu maalum katika hospitali ya Muhumbili baada ya kushikwa na a na maradhi wiki kadhaa zilizopita.

Taarifa kutoka Bongo zinasema kuwa rapa huyo ambaye amekuwa akitumbuiza kwa miaka mingi na pia kuhudumu kama mbunge alilazwa takriban wiki tatu zilizopita akiwa hali mahututi.

Wiki chache zilizopita Familia na marafiki wa Jay sasa walitoa wito wa msaada wa kifedha kutoka kwa wasamaria wema ili kugharamia matibabu yake.

Nyota wa nyimbo za injili Rose Muhando, kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amemtakia Jay afueni ya haraka.

Hata hivyo msanii huyo alimweleza kwamba mika miwili iliyopita alipitia aliyoyapitia, lakini Mungu alikuwa mwaminifu kwake kwani ni Mungu wa upendo.

Pia Rose alitoa mfano wa Ayubu ambaye alijaribiwa na magonjwa na kudao kwamba magonjwa sio mipango ya Mungu bali ya shetani.

"Magonjwa sio mpango wa Mungu bali ni hila za shetani ndio maana hata Ayubu alijaribiwa na shetani kupitia magonjwa na kwasababu sisi ni Binadamu kuugua ni ibada, inatukumbusha kwamba Mungu yupo na tunapaswa kumshukuru kwa kuendelea kutupa uhai kila iitwayo leo, hali unayoipitia niliwahi ipitia miaka miwili iliyopita lakini kwa sababu namuamini sana Mungu niliivuka, nakuombea sana @professorjaytz Mungu wetu ni waupendo na kwakua tunamwamini basi utapona," Aliandika Rose Muhando.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved