logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Inasikitisha Keroche imefungwa- Anerlisa Muigai azungumza

Sisi (Kampuni ya Nero) tunaishi nao kiwanja kimoja na niseme, imesikitisha sana kuona Keroche imefungwa

image
na Radio Jambo

Habari05 March 2022 - 10:47

Muhtasari


  • Mrithi wa Keroche Anerlisa Muigai amezungumza kuhusu jinsi kufungwa kwa kiwanda hicho kunavyoathiri biashara yake Nero Company

Mrithi wa Keroche Anerlisa Muigai amezungumza kuhusu jinsi kufungwa kwa kiwanda hicho kunavyoathiri biashara yake Nero Company.

"Inasikitisha sana kwamba Keroche imefungwa na hakuna mtu anayeonekana kutaka kusikiliza, kusaidia au kujadiliana," Anerlisa alisema katika taarifa aliyochapisha kwenye hadithi zake za Instagram.

"Sisi (Kampuni ya Nero) tunaishi nao kiwanja kimoja na niseme, imesikitisha sana kuona Keroche imefungwa kwa miezi miwili na mbaya zaidi, takriban watu 650 wamekwama wakishangaa ni lini Keroche itaanza kufanya kazi na pia hatari ya kupoteza kazi zao," aliongeza.

Anerlisa alibainisha, "Kila wakati ninajiuliza ikiwa kwa vyovyote vile kampuni kubwa kama Keroche inaweza kufungiwa hivyo sisi na biashara zingine zijazo tunapataje nguvu ya kuendelea? kuendesha biashara zetu?"

Aliendelea,

"Unapataje kodi zako kwa kufunga Keroche na juu ya hayo unaziambia benki zote zisiwape mkopo. Mtu anaweza kupata unyama kiasi gani? Kwa wakati huu, nitamwachia Mungu kila kitu. Mei Mungu atusaidie sote."

Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Keroche, Tabitha Karanja alichapisha taarifa akielezea hasara ambayo kampuni hiyo itapa baada ya kufungwa.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved