logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baby mamas wa Diamond, Hamisa Mobetto na Tanasha waonyeshana upendo mkubwa

Licha ya kuwa waliwahi kuwa na mahusiano na Diamond, Hamisa na Tanasha wameonyeshana upendo mkubwa

image
na SAMUEL MAINA

Burudani04 April 2022 - 10:18

Muhtasari


  • •Mobetto ambaye pia ana mtoto mmoja na Diamond ni miongoni mwa wanamitandao waliomsherehekea Tanasha na mwanawe.

Baby mamas wawili wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto na Tanasha Donna wamethibitisha wazi kwamba hakuna uhasama wowote kati yao.

Licha ya kuwa wote waliwahi kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na Diamond, Hamisa na Tanasha wameonyeshana upendo mkubwa kupitia mtandao wa Instagram.

Siku ya Jumapili, Tanasha alipakia picha yake na mwanawe anayefanana na Diamond kama shilingi kwa ya pili, Naseeb Juniour.

Mobetto ambaye pia ana mtoto mmoja na Diamond ni miongoni mwa wanamitandao waliomsherehekea Tanasha na mwanawe.

"Bi Ayyksha❤️😍," Mobetto aliandika chini ya chapisho la Tanasha.

Tanasha hakusita kujibu ujumbe wa Mobetto huku akimthibitishia kuwa anampenda.

"Nakupenda🥰," Tanasha alimjibu Mobetto.

Mwanasoshalaiti Huddah Monroe na mwanamuziki kutoka Nigeria Omah Lay ni baadhi ya wanamitandao wengine waliowasherehekea Tanasha na Naseeb Jnr.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved