logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lilian Ng'ang'a awasuta vikali watu maarufu wanaomezea mate nyadhifa za kisiasa

Lilian amesema watu kama hao kwa kawaida huwa hawana maslahi ya watu moyoni.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri12 April 2022 - 19:53

Muhtasari


•Mke huyo wa zamani wa gavana Alfred Mutua amesema watu kama hao kwa kawaida huwa hawana maslahi ya watu moyoni.

•Lilian amesema hatua ya watu kuwania viti kwa sababu ya umaarufu wao ni jambo la kusikitisha na kudai kuwa ni kiki tu.

Aliyekuwa mpenzi wa gavana Mutua Lilian Ng'ang'a

Bi Lilian Ng'ang'a amewakosoa watu mashuhuri ambao wanajitosa kwenye siasa na kuwania nyadhifa mbalimbali.

Mke huyo wa zamani wa gavana Alfred Mutua amesema watu kama hao kwa kawaida huwa hawana maslahi ya watu moyoni.

"Kwa sababu mtu ni maarufu (kwa sababu yoyote ile) haimaanishi agombee wadhifa. Wengi kama hao hawana nia ya kuwatumikia watu," Lilian alisema kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Lilian amesema hatua ya watu kuwania viti kwa sababu ya umaarufu wao ni jambo la kusikitisha na kudai kuwa ni kiki tu

"Ni kutafuta kikitu.  Inatisha," Alisema.

Lilian alimtema gavana Mutua mwaka jana baada ya kuwa pamoja kwa takriban mwongo mmoja. Kwa  sasa yupo kwenye ndoa nyingine na mwanamuziki Julius Owino almaarufu Juliani.

Juliani anajulikana kuwa mkosoaji wa serikali na tayari amewahi kutoa nyimbo kadhaa akilalamikia uongozi mbaya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved