logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nimepitia mengi, naskia kupumzika na kubarikiwa-Anerlisa Muigai

Aidha Anerlisa amekiri kwamba anajihisi akiwa na amani, na kupendwa.

image
na Radio Jambo

Habari16 April 2022 - 21:54

Muhtasari


  • Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram alisema kwamba amepitia mengi, na kwamba kwa sasa anahisi kwamba amebarikiwa
Mrithi wa Keroche, Anerlisa Muigai

Mfanyibiashara Anerlisa Muigai alifahamika sana mitandaoni baada ya kufunga pingu za maisah ya msanii kutoka Tanzania Ben Pol.

Pia alivuma mitandaoni baada ya kumpoteza dada yake Tecra.

Mama ya Anerlisa alishinda tikiti ya UDA katika uteuzi wa useneta wa Nakuru, huku imlazimu kumwandikia ujumbe wa kipekee.

Baada ya Anerlisa kutalikiana na mumewe, anaonekana kuendelea na maisha yake huku akijitosa kwenye biashara.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram alisema kwamba amepitia mengi, na kwamba kwa sasa anahisi kwamba amebarikiwa.

"Siku ya leo ni moja wapo wa siku ambazo naweza sema naskia nimepumzika na kubarikiwa nimepitia mengi, kumpoteza da yangu, talaka,biashara ya familia kuathiriwa na kukabiliana na kuvamiwa," Aliandika Anerlisa.

Aidha Anerlisa amekiri kwamba anajihisi akiwa na amani, na kupendwa.

"Sasa najihisi nina amani, kupendwa na kupata motisha zaidi, kila kitu kinafanyika kwa sababu zake na kwa maombi kila kitu kinafanyika kwa wakati wake kuna mwanagaza mwishoni mwa handaki."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved