logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamume hutulia pale anapopata amani,sio urembo-Mejja

Pia msanii huyo alisema kwamba sio pesa wala urembo unaomfanya mwanamume kukaa

image
na Radio Jambo

Habari04 May 2022 - 09:17

Muhtasari


  • Lakini sababu kuu ya uhusiano wa kimapenzi kutodumu katika karne hii ya sasa ni ipi?

Msanii Mejja ni mwanamuziki ambaye anafahamika sana Afrika Mashariki kutokana na bidi ya kai yake ya usanii.

Mejja ni miongoni mwa wasanii ambao wamesalia katika tasnia ya muiki kwa muda mrefu sasa, huku wakionyesha bidii yao kila siku.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram, amepakia ujumbe kuhusu wanaume, huku akiamini kwamba mwanamume hukaa kwenye uhusiano wa kimapenzi kutokana na amani ambayo anapokea.

Pia msanii huyo alisema kwamba sio pesa wala urembo unaomfanya mwanamume kukaa kwenye uhusiano wa kimapenzi.

"Mwanamume hutulia mahali anapata amani,sio urembo,sio pesa wala sio cheo bali amani," Aliandika Mejja.

Tumewaona wengi wakitangaza uhusiano wao wa kimapenzi mitandaoni huku baada ya muda mchaceh wanaachana,huku wengi wao wakitalikiana kwa jambo moja au nyingine.

Lakini sababu kuu ya uhusiano wa kimapenzi kutodumu katika karne hii ya sasa ni ipi?

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved