logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nilipata mapenzi ya kweli,'Jacque Maribe asherehekea siku ya kuzaliwa ya mwanawe

Mwanawe Jacque, na mcheshi Eric Omondi Zahari anaadhimisha miaka 8 hii leo.

image
na Radio Jambo

Habari14 May 2022 - 06:37

Muhtasari


  • Jacque Maribe asherehekea siku ya kuzaliwa ya mwanawe
  • Pia Maribe akimsherehekea mwanawe amesema kwamba baada ya kumpata mwanawe alipata mapenzi ya ukweli

Ni furaha ya kila mama kumuona mwanawe au wanawe wakikua kila siku, na kukua kutoka kiwango kimoja hadi kingine.

Hawakukosea kusema kwamba watoto ni baraka kwa kila mtu, ila kuna wale wana tabia ya kuavya mimba ili waweze kuonekana wazuri.

Aliyekuwa mwanahabari wa runinga ya Citizen Jacque Maribe, huku akisherehekea siku ya kuzaliwa na mwanawe amesimulia jinsi, mwanawe aliweza kubadilisha maisha yake.

Pia Maribe akimsherehekea mwanawe amesema kwamba baada ya kumpata mwanawe alipata mapenzi ya ukweli.

Mwanawe Jacque, na mcheshi Eric Omondi Zahari anaadhimisha miaka 8 hii leo.

"Miaka 8 iliyopita leo, maisha yangu kama nilijua yalibadilika kabisa, na kuwa bora. Kichwa kipya, nilipata upendo wa kweli, nilipata kusudi na maana. Nikawa mama, mara mama Zahari. Na nimeipenda kila dakika ya safari hii.

Zahari - maana yake Mungu Amekumbuka. Nisingeweza kukuchagulia jina bora mwanangu. Na kupitia safari yetu, Mungu amekumbuka kwa uaminifu.

Nakupenda kuliko maneno yote katika vitabu vyote katika ulimwengu mzima.

Heri ya miaka 8 ya kuzaliwa, King Zee!!,"Aliandika Jacque.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved