logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Utakumbukwa milele na daima" Omosh amuomboleza baba yake

Omosh alisema babake atakumbukwa zaidi kutokana na nyakati nzuri ambazo alishiriki nao.

image
na Radio Jambo

Burudani05 June 2022 - 17:35

Muhtasari


•Omosh alitangaza kuhusu kifo cha mzazi huyo wake Jumapili na kumtaja marehemu kama mtu mzuri ambaye atakumbukwa milele.

•Marehemu pia ni baba ya muigizaji mkongwe Naomi Kamau ambaye aliigiza kama mama ya Tina na Mike katika kipindi cha Mother-in-Law.

Muigizaji Joseph Kinuthia almaarufu Omosh kutokana na kipindi cha Tahidi High yupo katika hali ya kuomboleza baada ya kufiwa na babake mzazi.

Omosh alitangaza kuhusu kifo cha mzazi huyo wake Jumapili na kumtaja marehemu kama mtu mzuri ambaye atakumbukwa milele.

Huku akimtakia mapumziko ya amani Omosh, alisema babake atakumbukwa zaidi kutokana na nyakati nzuri ambazo alishiriki nao.

"Utakumbukwa milele na milele. Matukio mazuri uliyoshiriki nasi daima yatazungumza juu ya mtu bora ambaye ulikuwa. Pumzika kwa amani Baba," Omosh alisema kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Mchekeshaji huyo aliambatanisha ujumbe wake na picha inayoonyesha akiwa amemshika mzazi huyo wake kwenye bega.

Marehemu pia ni baba ya muigizaji mkongwe Naomi Kamau ambaye aliigiza kama mama ya Tina na Mike katika kipindi cha Mother-in-Law.

Haya yanajiri katika kipindi ambapo Omosh ameanza kufufua taaluma yake ya usanii baada ya kuwa amezama kwenye uraibu wa pombe kwa muda mrefu.

Katika mahojiano ya hapo awali muigizaji huyo alifichua kuwa alikuwa ameathirika na uraibu wa pombe kwa takriban miongo miwili.

"Nilikuwa mraibu kwa takriban miaka 20. Wakati huo singeweza kula ama kunywa chai asubuhi kama sijachomwa. Asubuhi nikiamka ningetoa sababu yoyote ili nitoke kwa nyumba ndio niende nikakunnywe," Omosh alisema akiwa kwenye mahojiano na Grace Makena.

Alisema alikaa miaka minne bila kuonja mvinyo baada ya kupelekwa rehab. Hata hivyo janga la Corona lilipokumba dunia alijipata kwenye majaribu na kuanza kulewa tena na hapo masaibu zaidi yakaanza.

Siku kadhaa zilizopita muigizaji huyo alihudhuria ibada katika kanisa la mhubiri mashuhuri Victor Kanyari ambaye aliombea taaluma yake na kumkabidhi zawadi kemkem.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved