logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ikitokea nimekufa bendera ya Tanzania haipo-Diamond ajisifia kuwa mwanamuziki bora Tanzania

Nambari mbili ni Davido, tatu Ckay, nne Diamond Platnumz na tano Kizz Daniel

image
na Radio Jambo

Yanayojiri24 June 2022 - 12:58

Muhtasari


  • Huwa anajitaja kuwa bora zaidi nchini Tanzania, Afrika Mashariki na hata Afrika nzima

Staa wa bongo Diamond Platnumz ni mwanamuziki wa Tanzania na muziki wake umeenea sehemu mbali mbali ulimwenguni.

Huwa anajitaja kuwa bora zaidi nchini Tanzania, Afrika Mashariki na hata Afrika nzima.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amerudia hilo ambapo alichapisha orodha iliyoandaliwa na Innocent Mjagi Kwenye Twitter ya wasanii kumi wa Afrika ambao Wana ushawishi mkubwa ulimwenguni.

Orodha hiyo imejaa wasanii wa Nigeria ambao wamechukua nafasi 8 na nyingine mbili zilizosalia ni za Diamond Platnumz na Fally Ipupa wa Congo.

Nambari mbili ni Davido, tatu Ckay, nne Diamond Platnumz na tano Kizz Daniel. Olamide, Fireboy, Rema, Fally Ipupa na Tems wanakamilisha orodha hiyo.

Baada ya kupakia orodha hiyo, mwanamuziki huyo amedai iwapo ataaga dunia leo, bendera ya Tanzania ya burudani haitakuwepo kwenye orodha hiyo.

“Kiufupu ikitokea nimekufa bendera ya Tanzania haipo hapo pengine top 100 Inshallah,"Aliandika Diamond.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved