logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hisia mseto baada ya Omosh kuonekana kwenye uzinduzi wa Manifesto ya Wajackoyah

Omosh alikuwa amevalia shati nyeupe iliyochorwa picha ya Wajackoyah na kauli mbiu 'Uhuru Unakuja.'

image
na Radio Jambo

Habari01 July 2022 - 11:48

Muhtasari


  • Hisia mseto baada ya Omosh kuonekana kwenye uzinduzi wa Manifesto ya Wajackoyah

Mwigizaji  maarufu Joseph Kinuthia almaarufu Omosh amevutia hisia za wengi baada ya kuonekana wakati wa uzinduzi wa manifesto ya Roots Party of Kenya mnamo Alhamisi Juni 30.

Omosh alikuwa amevalia shati jeupe liliyochorwa picha ya Wajackoyah na kauli mbiu 'Uhuru Unakuja.'

Muigizaji huyo wa zamani wa Tahidi High hapo awali aliahidi utiifu kwa chama cha William Ruto cha United Democratic Alliance (UDA) lakini uwepo wake katika manifesto ya Wajackoyah iliyozinduliwa ulionekana kufichua kuwa Omosh alikuwa amebadili upande wake.

Picha zake akiwa na rangi za UDA na rangi za Roots Party of Kenya zimezua hisia tofauti kutoka kwa Wakenya kwenye mitandao ya kijamii.

Haya yanijiri mieezi chache baada ya mwigizaji huyo kutangaza rasmi kwamba amejiunga na chama cha UDA.kinachoongozwa na naibu rais William Ruto.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved