logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ujumbe wa Ekodydda kwa wafuasi wake baada ya kuripotiwa kupigwa na kutekwa nyara

Eko alibainisha kuwa mpinzani wake mkuu amekuwa akitumia majambazi kurejesha uongozi

image
na Radio Jambo

Yanayojiri12 August 2022 - 20:27

Muhtasari


  • Aliweka wazi kuwa hatawaruhusu wahuni wachache ambao hawaheshimu matakwa ya watu huko Mathare Kaskazini kumnyima ushindi, akiongeza kuwa kura lazima zihesabiwe wakati huu
Ekodydda

Rapa maarufu wa nyimbo za injili Ekodydda amesema hataogopa vitisho baada ya kudaiwa kuvamiwa na kutekwa nyara na wapenzi wa mpinzani wake baada ya kutangazwa mshindi wa Wadi ya Mathare Kaskazini.

Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram saa chache baada ya kuripotiwa kutoweka, rappa huyo aliyegeuka kuwa mwanasiasa alisema atafanya kila awezalo ili kurudisha cheti chake.

Aliweka wazi kuwa hatawaruhusu wahuni wachache ambao hawaheshimu matakwa ya watu huko Mathare Kaskazini kumnyima ushindi, akiongeza kuwa kura lazima zihesabiwe wakati huu.

Eko alibainisha kuwa mpinzani wake mkuu amekuwa akitumia majambazi kurejesha uongozi wake mbovu, jambo ambalo ameahidi kulipigania hadi mwisho.

''Nitajitahidi niwezavyo kurudisha cheti changu, ni rahisi, hatuwezi kuwaachia wahuni wachache kuendelea kulazimisha kata nzima kusaga uongozi mbaya. Kwa nini watu wanapiga kura ikiwa kura zao hazitahesabiwa? Ninawaahidi Wadi ya Mathare Kaskazini kwamba kura zenu lazima zihesabiwe mara hii,’’ aliandika.

Hapo awali, mke wa Ekodydda Cynthia Ayugi alikuwa ametangaza kwa umma kwamba ametoweka.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved