logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sonko ataka watu wamuombee aache pombe, apakia video ya Ruto akiimba

“Nimeguswa na Rais wetu mpaka najiskia kuokoka, ikulu ya sherehe sasa yageuka kuwa hekalu ya maombi,”alisema.

image
na Radio Jambo

Habari26 September 2022 - 13:07

Muhtasari


• Tajiri huyo aliwataka wafuasi wake pia kumtia katika maombi ili naye apate kuokoka na kuacha kutumia pombe.

Sonko amesema ikulu imebadilika na kuwa sehemu takatifu

Sonko alisema kwa mshangao kuwa Rais wa sasa ameweza kuibadilisha ikulu ikawa mahali pa maombi,

Kiongozi huyo alipakia video ya rais Ruto akifanya ibada kwenye ikulu huku akiwa miongoni mwa watu waliokuwa wakiimba kwa kusujudu.

Tajiri huyo aliwataka wafuasi wake pia kumtia katika maombi ili naye apate kuokoka na kuacha kutumia pombe, kwa kusema kwamba baada ya kupata wokovu atakuwa anakunywa kidogo kama Yesu.

"Niombeeni niwache pombe na kama ni kukunywa niwe nakunywa kidogo kidogo kama ile mvinyo ambayo Yesu alikuwa anakunywa. Yuko Mungu mbinguni asikuaye maombi," Sonko aliandika kwa utani wa aina yake.

Sonko anatoa matamshi haya siku moja tu baada ya rais Ruto na familia yake kuandaa ibada kubwa kabisa katika ikulu ya Nairobi ambapo aliwarai viongozi hao wa kanisa kuzidi kuliweka taifa mikononi mwa bwana.

Ibada hiyo iliyohudhuriwa na viongozi wa kanisa zaidi ya 40 ilikuwa pia imeandaliwa kuuombea uchumi na migororo ambayo imekuwa ikikumba taifa la Kenya.

"Nawataka muombee amani ya nchi yetu. Kenya ni nchi tegemeo. Nilizungumza na viongozi wengi kwa muda wa wiki kadhaa zilizopita na wanaangalia Kenya ili kutoa suluhu kwa amani ya eneo letu. Kutoka Somalia hadi Ethiopia. Hadi DRC ,Sudan Kusini na eneo lote hili,” alisema.

Mama wa Taifa Rachel Ruto pia aliongelea suala hilo la kutakasa Ikulu.

Alisema kuwa Ikulu itakuwa mahali pa maombi ambapo ibada itakuwa ikiandaliwa kila mwezi kwa minajili ya kutoa shukrani kwa Mwenyezi Mungu.

Ibada hiyo iliyoandaliwa katika Ikulu ya Nairobi ndiyo ya kwanza kufanyika kutoka uapisho wake Rais na baada yake kuhamia kule Ikuluni. Iliwakutanisha viongozi mbali mbali wa Kikristo waliojumuika kufanya maombi maalum.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved