logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Siwezi amini ameaga dunia,'Alinur amuomboleza rapa Takeoff

Takeoff aliripotiwa kuuawa baada ya kupigwa risasi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri01 November 2022 - 16:43

Muhtasari


  • Baadaye Takeoff alipelekwa katika hospitali kuu ya Georgia baada ya kuzirai na baadaye kutambulika kuwa amefariki

Mwanasiasa na mfuasi sugu wa Azimio Mahamed Alinur, kupitia kwenye ukurasa wake rasmi wa twitter amemuomboleza  Rapa wa kikundi cha Amerika cha Migos, Takeoff.

Takeoff aliripotiwa kuuawa baada ya kupigwa risasi.

Kulingana na ripoti za Amerika,rapa huyo alikuwa amemtembelea rafiki yake kwa likizo zilizokuwa kabla ya kupigwa risasi  Billiard and Bowling huko Houston. .

Alikuwa na mjomba na mwanachama mwenza wa Migos, Offset pamoja na wasanii wa rapa wa Atlanta Young Thug na 21 Savage wakati kisa hicho kilipotokea.

Kundi hilo lilikuwa kwenye gari katika harakati zao kisha kuhudhuria sherehe ya rafiki yao Jas Prince kabla ya kuuliwa.

Kulingana na Hollywood Unlocked na wengine, Offset alidai kuwa gari lingine liliwazuia kuendelea na safari yao na kufyatua risasi.

Baadaye Takeoff alipelekwa katika hospitali kuu ya Georgia baada ya kuzirai na baadaye kutambulika kuwa amefariki.

"Siamini kwamba Takeoff kutoka kwa wana hip hop watatu wa Marekani Migos amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na kuuwawaMaombi yangu kwa familia yake, Quavo, Offset na Marafiki. lala salama Takeoff,"Aliandika Alinur.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved