logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Inauma!" Willis Raburu amuomboleza mwanafamilia wa karibu

Raburu alifichua kwamba ameridhi jina la marehemu na kwa hilo akaahidi kuendelea kuliheshimisha siku zote.

image
na Radio Jambo

Habari17 February 2023 - 06:58

Muhtasari


•Raburu alitangaza kifo cha babu yake, Ker Willis Opiyo Otondi siku ya Ijumaa asubuhi na kusema kwamba ni pigo kubwa kwake na inauma.

•Raburu alifichua kwamba ameridhi jina la marehemu na kufuatia hilo akaahidi kuendelea kuliheshimisha siku zote.

ameaga dunia

Mtangazaji na mburudishaji maarufu Willis Raburu yuko katika hali ya maombolezo.

Raburu alitangaza kifo cha babu yake, Ker Willis Opiyo Otondi siku ya Ijumaa asubuhi na kusema kwamba ni pigo kubwa kwake na inauma.

"Inawezekanaje lakini eti jana tu tulikuwa tunazungumza na leo ..."  aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Aliambatanisha ujumbe wake na picha kadhaa za kumbukumbu za marehemu ambaye alionekana katika miaka ya uzeeni.

Willis alimkumbuka Bw Opiyo kama mtu mwenye kuzungumza mawazo  yake, mkali na mwenye furaha na tabasamu nzuri.

"Ulisimama kidete. Ulitujali sote na ulitaka kuhusika katika maisha yetu," Willis alisema kuhusu marehemu.

Mtangazaji huyo alifichua kuwa babu yake alikuwa mwenyekiti wa baraza la wazee wa Kijaluo na kusema matendo yake wakati akitumikia nafasi hiyo yatakumbukwa daima.

Pia alifichua kwamba ameridhi jina la marehemu na kufuatia hilo akaahidi kuendelea kuliheshimisha siku zote.

"Ninaishi kuheshimu urithi na kumbukumbu yako kwa kutangaza jina lako! Nimebarikiwa na kuheshimiwa kuendelea na jina Willis Edwin Opiyo Otondi,"

Willis alimtakia babu yake mapumziko ya amani na kusema  kwamba atamkosa sana.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved