Unakaa pasta Ng'ang'a-Sonko aambiwa baada ya kupakia picha yake ya zamani

Zaidi ya yote Sonko alimshukuru Mungu kwa kumpa fursa nyingine ya kuongeza mwaka mwingine.

Muhtasari
  • Kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram alipakia picha hiyo na kuiambatanisha na ujumbe huku akisimulia changamoto alizopitia nyakati zile.
Aliyekuwa gavana wa Nairoi, Mike Sonko
Aliyekuwa gavana wa Nairoi, Mike Sonko
Image: Facebook//Mike Sonko

Aliyekuwa gavana wa Naironi Mike Sonko  anasherehekea siku yake ya kuzaliwa hii leo.

Sonko alishiriki picha yake ya zamani ambapo wanamitandao wengi wametooa hisia tofauti huku baadhi yao wakimtakia heri njema ya kuzaliwa.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram alipakia picha hiyo na kuiambatanisha na ujumbe huku akisimulia changamoto alizopitia nyakati zile.

Zaidi ya yote Sonko alimshukuru Mungu kwa kumpa fursa nyingine ya kuongeza mwaka mwingine.

"Nimepitia nyakati nzuri na ngumu. Ninafurahi kwamba, kupitia heka heka, bado nimesimama kidete. Lakini katika yote, ninamshukuru Mungu kwamba niko hai ili kushuhudia wema wake kwa wote. Asante Mungu kwa kunijaalia mwaka mwingine wa maisha yangu. Bwana, ninakuombea uniongoze, unisamehe dhambi zangu na uniruhusu niishi maisha yangu kwa furaha. Upendo wa Kimungu na rehema zote ninakuuliza, Mungu wangu mpendwa. Heri ya kuzaliwa kwangu, mimi mwenyewe na mimi,"Alisema Sonko.

Wanamitandao wengi walionekana kufurahiswa tu na picha ya Sonko, na hizi hapa baadhi ya hisia zao;

iamlavalava: Happy birthday To you long Life @mike.sonko

he.babuowino: Happy birthday @mike.sonko operations.May God grant you the best health.

supreme___kimani: Hapa unakaa pastor nganga

moskyalo: Looks like he's holding a face mask. By then I don't think we knew about face mask.

ombimavoh: Happy birthday Mhesh, kujituma hulipa na there is no permanent situation. GOD BLESS YOU ON YOUR SPECIAL 🙌🙌🔥

patokmjunior: Whaat! Kama huyu ni wewe Mhesh" basi sina haraka na life ya kuomoka tena!

rapudosallie: Happiest birthday nlikuona city mall nkatakamani kukusalimia nkaogopa squad😂😂😂