logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nahitaji msaada!,'Mc Fullstop azungumza baada ya kudaiwa kufariki

"Hii imeenda” kwa kweli. Pafu langu la kushoto limeanguka kabisa nimebaki na moja,"

image
na Radio Jambo

Burudani12 May 2023 - 14:32

Muhtasari


  • Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa imeripotiwa kuwa mshukiwa huyo alitumia nembo ya Citizen TV Kenya kudai kuwa Mc huyo mashuhuri amefariki dunia.
  • Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Mc fullstop, alidai kuwa anakwenda kumchukulia hatua mtuhumiwa huyo.

Mtangazaji mashuhuri wa Reggea, John Maina almaarufu MC Fullstop ameomba usaidizi wa kumtafuta mshukiwa ambaye amekuwa akidai kuwa amefariki.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa imeripotiwa kuwa mshukiwa huyo alitumia nembo ya Citizen TV Kenya kudai kuwa Mc huyo mashuhuri amefariki dunia.

Akitumia akaunti zake tofauti za mitandao ya kijamii kutoa maoni yake kuhusu mada hii, MC FULLSTOP amemtaja mwanamume huyo ambaye alisema amekuwa akifanya hivyo kwa muda.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Mc fullstop, alidai kuwa anakwenda kumchukulia hatua mtuhumiwa huyo.

"Amenizuia tu! Ila bado tunaweza kumpata, sio first time nimefanya hivi but saa hii ame affect my whole family, wameshtuka, panic wazee ndio mmeathirika sana. @DCI_Kenya@NPSOfficial_KE@PolisiKE NAHITAJI MSAADA!" Aliongea Fullstop.

Wakati wakijibu kisa hicho, Wakenya waliotumia akaunti zao tofauti za mitandao ya kijamii kutoa maoni yao kuhusu madai haya wameitaka idara ya upelelezi wa makosa ya jinai kumsaidia DJ huyo kumpata mshukiwa.\

Mwezi mmoja uliopita Mtangazaji huyo maarufu wa nyimbo za Reggea na Dancehall alibainisha kwamba anapata shida sana kukimbia, kutembea na hata kuzungumza baada ya ugonjwa huo kuathiri mapafu na koo lake.

"Hii imeenda” kwa kweli. Pafu langu la kushoto limeanguka kabisa nimebaki na moja," alisema kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Aliongeza, "Mwaka wa 2021 niligunduliwa na TB ya mapafu ikakula mapafu kabisa. 2022 nikapata TB ya koo nayo ikanimaliza sauti. Kukimbia, kutembea na kuongea ni shida,"

Maina aliambatanisha ujumbe huo na picha yake akiwa amelala kwa kitanda cha hospitali huku akiwa anawekwa hewa kupitia mrija ambao uliwekwa kwenye pua lake na picha nyingine ya X-ray iliyoonyesha jinsi pafu lake limeathirika.

Alidokeza kwamba hajisikii sawa na kuwashukuru wale ambao wamekuwa wakisimama naye wakati wa ugonjwa wake.

"Alafu mapafu yana ufala sio kama ini, haiwezi kujiponya itabidi nijipange hapa naona niki hang boots. Nataka tu kusema asante kwa wale wamekuwa wakinisapoti katika kipindi hiki kigumu Mungu awabariki sana," alisema.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved