logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Manzi wa Kibera amtema mchumba wake mzee, afichua sababu

Mwanasoshalaiti huyo alisema wanamitandao walimuonyesha chuki huku wengine wakimrushia cheche za matusi.

image
na Davis Ojiambo

Burudani19 May 2023 - 08:03

Muhtasari


  • • Manzi wa Kibera aliyeonekana kujawa na huzuni alitangaza kuwa yeye na mzee hawako pamoja tena.

Mwanasoshalaiti Sharifa Sharon Wambui almaarufu Manzi wa Kibera amefichua ametengana na mchumba wake mzee.

Kwenye instastori zake, Manzi wa Kibera aliyeonekana kujawa na huzuni alitangaza kuwa yeye na mzee hawako pamoja tena.

"Mimi na mzee hatuyuko pamoja tena," alisema mwanasosholaiti huyo na kumalizia kwa emoji za huzuni.

Mmoja kati ya mashabiki yake alimuuliza sababu ya kutengana na mzee na akaeleza kwamba ataelezea zaidi baadaye kwa kuwa ni hadithi ndefu.

Mwanasoshalaiti huyo alielezea kuwa amewaza kuvunja mahusiano na mpenzi huyo wake wa miaka 66 kutokana na chuki na unyanyasaji iliyoko mtandaoni.

Aliendelea kueleza kuwa wanamitandao wengi walimuonyesha chuki huku wengine wakimrushia cheche za matusi katika sehemu ya maoni na alisema kuwa watu wengi walikuwa wakipinga uhusiano wake na mchumba wake mzee.

Wiki chache zilizopita, katika video zilizovuma kwenye mitandao ya kijamii, mwanasosholaiti huyo asiyepungukiwa na drama alionekana akiwa ameandamana na mpenziwe kabla ya mzee huyo kupiga magoti na kumuomba wafunge ndoa.

Baadaye, mwanasosholaiti huyo alidokeza kufunga pingu za maisha na mchumba huyo wake katika siku za hivi karibuni.

Licha ya kuchumbiana kwa muda mrefu, kipusa huyo anayezungukwa na sarakasi nyingi maishani hata hivyo amebainisha kwamba anasubiri ndoa rasmi ili kumuonjesha mchumba huyo wake zawadi ya ndoa aliyomhifadhia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved