logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mashabiki wapagawa Raila akiwahutubia live kutoka kwa akaunti ya TikTok ya Nyako

“Ninapenda TikTok na ninawapenda ninyi watu. Nimefurahi sana kuwafanya marafiki.' Raila alisema.

image
na Davis Ojiambo

Burudani03 November 2023 - 05:46

Muhtasari


  • • "Huyu ni Baba anazungumza na nyinyi watu. Hamjambo?" Raila alianza hotuba yake.
Nyako na Raila

Maelfu ya wafuasi wa kinara wa muda mrefu wa upinzani Raila Odinga jioni ya Alhamisi walipata nafasi adimu ya kumsikiliza kinara huyo akiwahutubia kwa mara ya kwanza kupitia mtandao wa TikTok.

Odinga alitokea katika kipindi cha moja kwa moja kwenye TikTok ya Nyako na kuwazungumzia mashabiki wake ambao walionesha furaha ghaya.

Nyako alikutana na Raila katika eneo lililofanana na nyumbani kwake, naye akamgeukia kamera, jambo ambalo liliwaacha watu wengi waliokuwa kwenye video hiyo ya moja kwa moja wakishangilia sana.

"Huyu ni Baba anazungumza na nyinyi watu. Hamjambo? Nina hapa binti mmoja ambaye amekuja kutoka Ujerumani ambaye ananiambia kuwa yeye ni bingwa wa TikTok na kwamba nahitaji kuzungumza na watazamaji kwenye TikTok.”

“Ninapenda TikTok na ninawapenda ninyi watu. Nimefurahi sana kuwafanya marafiki. Natumai tunaweza kutembea pamoja na kwa pamoja tutafanikiwa. Tutashinda. Aluta continua,” alisema.

Baba alikuwa amevalia shati la bluu bahari; alizungumza na kamera na pia akaendelea kumwangalia Nyako aliyekuwa amesimama nyuma ya simu, mwanasiasa huyo mkongwe akipata raha na mashabiki wake kupitia video ya moja kwa moja ya shabiki mwingine.

Tazama video hii hapa,


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved