Sandra Dacha azungumzia anachokienzi katika mapenzi

Dacha alitaja mahususi kuhusu watu mashuhuri wa Kenya ambao hangewahi kufikiria kuwachumbia.

Muhtasari
  • Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake na mcheshi mwenzake Akuku Danger, Dacha alikwepa jibu la moja kwa moja, na hivyo kuchochea uvumi kuhusu hali yao.
Muigizaji Sandra Dacha akiwa amejiweka vizuri kwa ajili ya picha
Muigizaji Sandra Dacha akiwa amejiweka vizuri kwa ajili ya picha
Image: Facebook//Sandra Dacha

Mwigizaji wa Kenya na mtayarishaji maudhui Sandra Dacha ameangazia upendeleo wake wa uchumba na kufichua maarifa ya kuvutia kuhusu maisha yake ya kimapenzi.

Katika mahojiano na Dk. Ofweneke, Dacha alijadili aina yake ya mpenzi anayefaa na kufichua mawazo yake kuhusu kuchumbiana na watu mashuhuri wa Kenya.

Wakati wa mahojiano, Dacha alitaja mahususi kuhusu watu mashuhuri wa Kenya ambao hangewahi kufikiria kuwachumbia.

Aliwakataa kwa ucheshi waigizaji Dr.Ofweneke na Mejja kama wapenzi watarajiwa, akitaja ukubwa wa mwili wa Mejja kama kizuizi.

"Kamwe! Sasa uko na tumbo na niko na tumbo,tutafanya nini? Ninaipenda nyembamba, mrefu, mweusi na mwenye sura nzuri. Nikupeleke wapi ukiwa hauna sura nzuri? Siwezi kuchumbiana na Ofweneke au Mejja."

“Siwezi kuchumbiana naye, unajua dawa ya ballon ni sindano. Yeye ni mkubwa. Sipendi wanaume wanene. Nataka mtu nyembamba alafu anakaa tu hivi hivi. Si mwenye sura mbaya," alisema kwa utani.

Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake na mcheshi mwenzake Akuku Danger, Dacha alikwepa jibu la moja kwa moja, na hivyo kuchochea uvumi kuhusu hali yao.

Ingawa aliepuka kuthibitisha hali yao ya sasa ya uhusiano, Dk Ofweneke  alikisia  kwamba wanaweza bado kuwa pamoja kulingana na kusita kwa Dacha kujibu swali hilo.

Mnamo Machi 2023, Akuku Danger alithibitisha hadharani uhusiano wake na Sandra Dacha wakati wa kipindi cha Maswali na Majibu kwenye Instagram.

Akijibu swali la mashabiki kuhusu hali yao, Akuku alionyesha mapenzi kwa Dacha, akimtaja kama 'ride-or-Die' yake. Pia alidokeza uwezekano wa kuwa na wake wengi katika siku zijazo, akipendekeza kwamba uhusiano wao ulisalia kuwa imara.

Mapenzi kati ya Akuku Danger na Sandra Dacha yalianza kujulikana kwa umma mwaka wa 2022 Dacha alipofichua uhusiano wao wakati wa hafla ya kuchangisha pesa kwa ajili ya Akuku Danger.

Wakati huo, alifichua kwamba walikuwa wamechumbiana kwa mwaka mmoja, jambo lililoashiria maendeleo chanya  katika ushirikiano wao.

Licha ya uthibitisho wa awali wa  uhusiano wao, hali ya sasa ya mapenzi ya Akuku Danger na Sandra Dacha bado haijafahamika.

Kwa sasa, hakuna mhusika aliyetoa taarifa za uhakika kuhusu kuendelea au kuhitimisha uhusiano wao.