logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maombi maalum ya mtangazaji Gidi kwa binti yake Marie-Rose anapotimiza miaka 8

Mtangazaji huyo ameomba kwamba msichana huyo mdogo akue kuwa mtiifu na Mcha Mungu Mungu.

image
na Radio Jambo

Burudani21 May 2024 - 12:11

Muhtasari


•Gidi ametumia fursa hiyo kumtakia bintiye kheri ya siku ya kuzaliwa na kueleza upendo wake mkubwa kwake.

•Aliambatanisha taarifa hiyo na picha nzuri ya kumbukumbu yake na Marie-Rose wakiwa nchini Ufaransa.

Binti ya mtangazaji Joseph Ogidi almaarufu Gidi, Marie-Rose Ogidi anasherehekea siku yake ya kuzaliwa hivi leo, Mei 21.

Msichana huyo mdogo mrembo anayeishi na mama yake nchini Ufaransa anatimiza miaka minane.

Gidi ametumia fursa hiyo kumtakia bintiye kheri ya siku ya kuzaliwa na kueleza upendo wake mkubwa kwake. Pia ameomba kwamba msichana huyo mdogo akue kuwa mtiifu na Mcha Mungu Mungu.

"Ni siku ya kuzaliwa ya Marie-Rose, Kheri ya siku ya kuzaliwa NyarKanyamwa. Uzidi kuwa mtiifu na msichana anayemuogopa Mungu. Upendo mwingi ❤️🙏,” Gidi aliandika kwenye Instagram.

Aliambatanisha taarifa hiyo na picha nzuri ya kumbukumbu yake na Marie-Rose wakiwa nchini Ufaransa.

Mwanzoni mwa mwaka uliopita, mtangazaji huyo wa kipindi cha Gidi na Ghost asubuhi kwenye Radio Jambo alitumia likizo yake kutembelea familia yake nchini Ufaransa na kuwa na wakati mzuri na binti yake mdogo Marie-Rose ambaye bila shaka ana uhusiano wa karibu sana naye.

Gidi na bintiye walitengeneza kumbukumbu nzuri pamoja wakati wa kikao chake cha muda mfupi na alipokuwa akijiandaa kurejea Kenya, kwaheri yao haikuwa rahisi na iligeuka kwa kipindi cha kihisia kama alivyoonyesha mtangazaji huyo kwenye video.

"Kwaheri sio rahisi😫," Gigi aliandika chini ya video fupi aliyochapisha kwenye mtandao wa Instagram akimfahamisha bintiye kuwa anarudi Kenya na kumuaga kwaheri.

Kwenye video hiyo, Marie-Rose alionekana akiwezwa na hisia pindi tu baada ya baba yake kumuarifu kwamba anataka kuondoka ili kurudi nchini Kenya.

"Marie-Rose, narudi Kenya," Gidi anasikika akimwambia bintiye.

Punde baada ya kusema hayo, binti yake alijibu kwa 'Hapanaa' kubwa na kuweka sura ya uso inayoonyesha kwamba hakutaka aondoke.

Mtangazaji huyo alipomuuliza bintiye ujumbe wa mwisho kwake kabla ya kuondoka, Marie-Rose alijibu, "Nitakumiss."

Pia alimhakikishia malkia huyo mdogo kwamba angemkosa sana pia baada ya kuondoka. Wawili hao kisha walionekana wakikumbatiana kihisia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved