Karen Nyamu ajigamba kuhusu Samidoh kuwalipia watoto karo katika shule za Kimataifa

Katika hotuba yake, Seneta alitambua ni kiasi gani wabunifu wametoa fursa nyingi kuwawezesha kutafuta pesa.

Muhtasari

•Bi Nyamu alitoa mfano wa mzazi mwenza wake Samidoh ambaye analipia karo watoto wao kuhudhuria shule za kimataifa.

•Kwa Karen, hii ilimaanisha kuwa tasnia ya burudani ya Kenya ilikuwa na fursa za kunyakua na kufanikiwa pia.

Seneta Nyamu na mpenzi wake Samidoh
Image: SAMIDOH// INSTAGRAM

Ulinzi mkali uliashiria kuingia kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua kwenye hafla ya uzinduzi wa kipindi cha televisheni cha Bahati Empire mnamo Alhamisi, Juni 6.

Mwanasiasa huyo alipokelewa kama shujaa katika hoteli moja ya Nairobi ambapo aliungana na wapenzi Bahati na Diana Marua waliokuwa wakisubiri kumpokea kama Mgeni wao wa Heshima.

Pia miongoni mwa wageni mashuhuri alikuwa ni Seneta Mteule Karen Nyamu, ambaye alihutubia hadhara.

Katika hotuba yake, Seneta alitambua ni kiasi gani wabunifu wametoa fursa nyingi kuwawezesha kutafuta pesa.

Alitoa mfano wa mzazi mwenza wake Samidoh ambaye analipia karo watoto wao kuhudhuria shule za kimataifa.'

"Watoto wangu, watoto wangu wako katika shule za Kimataifa. Na shule hulipwo kwa ubunifu. Si mnajua baba ya watoto wangu? Na analipa International School. Bora zaidi nchini," aliongeza.

Kwa Karen, hii ilimaanisha kuwa tasnia ya burudani ya Kenya ilikuwa na fursa za kunyakua na kufanikiwa pia.

"Kwa hiyo nyie mna uwezo mkubwa sana Nyinyi ndio mnaweza kuwa mabwenyenye wa nchi. Sote tunaweza kutamani kuwa katika nafasi hiyo kwa sababu ya aina ya pesa mnazoweza kutengeneza"

Pia alisema Eddie Butita ni kiongozi wa tasnia ambaye anapaswa kuigwa.

"Usiende hapo kucheka na Rais na viongozi wetu wa enjoy. Una ajenda usisahau, na uendelee kusukuma hadi kila kitu kitimizwe kwa sababu mna viongozi wenye ari ambao mnafaa kutumia..”

Matukio mengi yalifanyika katika uzinduzi wa Kenya wa kipindi cha televisheni cha Bahati Empire mnamo Juni 6.