logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Akina mama waandamana kulalamikia ongezeko la kuibiwa wanaume na mipango ya kando

“Kumbatia ndoa ya wanawake wengi na mfurahie maisha yenu,” mwingine aliwaambia.

image
na Davis Ojiambo

Burudani10 June 2024 - 12:22

Muhtasari


  • •“Tunataka mwisho kwa kunyakuliwa kwa wanaume, ikiwa tutakukamata na mwanamume wa mwenyewe, nitakuanika mitandaoni,” kiongozi wa maandamano hayo alisema.
Wanawake waandamana kulalamikia kuibiwa wanaume

Baadhi ya wanawake walioolewa wamezua gumzo mitandaoni huku wakitoka nje kupinga kasi ya kutisha ya unyakuzi wa waume unaoendelea.

Video hiyo inadaiwa kurekodiwa katika soko moja katika jimbo la Asaba nchini Nigeria na makumi ya wanawake wanaodaiwa kuwa katika ndoa walionekana wakiandamana na mabango yenye jumbe za kuelezea mfadhaiko wao dhidi ya ongezeko la ‘mipango ya kando’ kuwanyakua wanaume wao.

Katika jumbe kwenye mabango yao, akina mama hao walionekana wakijiburuza na kujitupa sakafuni kwenye lami wakidai kwamba ongezeko la wanawake wasio na wanaume kuwachukulia wanaume wao limesababisha wanaume wengi kuishia kutowajibika katika familia zao, kwani mara nyingi rasilimali nyingi huishia midomoni mwa michepuko na familia kusalia kutelekezwa.

Moja ya bango walilokuwa wameshika lilisomeka; “Tumechoka. Wasichana wasio na waume tafadhali waache waume wa wenyewe ili warudi kwa wake zao na watoto wao.”

Waliapa kuwafichua wanawake wasio na waume ikiwa watawakamata na waume zao.

“Tunataka mwisho kwa kunyakuliwa kwa wanaume, ikiwa tutakukamata na mwanamume wa mwenyewe, nitakuanika mitandaoni,” kiongozi wa maandamano hayo alisema.

Video hiyo iliyochapishwa katika jukwaa la X ilivutia maoni kinzani na haya hapa ni baadhi ya maoni yenye mvuto;

“Baada ya kuwafukuza waume zao wenye tabia mbaya, wanawalaumu michepuko kuwa anawafanyia kazi zao 🤣” Chaxton alisema.

“Kumbatia ndoa ya wanawake wengi na mfurahie maisha yenu,” mwingine aliwaambia.

“Dawa pekee ya kumtunza mume ni kumtendea mema na kujitiisha chini ya ukichwa wake katika ndoa yenu. Mara tu nyumba inapokuwa na joto sana kwake, wasichana wengine watampa joto.”Jeff Onyedili.

Tazama video hapa;


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved