logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanasosholaiti Huddah Monroe afafanua maana ya profile picture yake mpya Instagram

Kwa muda mrefu, Huddah Monroe amekuwa akitumia picha ya Mzee Jomo Kenyatta.

image
na Davis Ojiambo

Burudani30 June 2024 - 06:47

Muhtasari


  • • Kwa muda mrefu, Huddah Monroe amekuwa akitumia picha ya rais wa kwanza na mwanzilishi wa taifa la Kenya Mzee Jomo Kenyatta.
Hoddah Monroe na profile pic mpya

Mwanasosholaiti wa muda mrefu Huddah Monroe amejipata kwenye kikaango cha maswali mengi kutoka kwa mashsbiki wake baada ya kubadilisha picha yake ya utambulisho kwenye Instagram na kutumia picha ya jicho.

Huddah, alilazimika kutoa ufafanuzi juu ya hilo, kutokana na baadhi ya mashabiki wake kumshinikiza kufanya hivyo wakidai kwamba picha ya jicho aliyoitumia inahusishwa na nguvu za gizani katika baadhi ya filamu za ughaibuni.

Hata hivyo, Huddah alieleza kwamba picha hiyo ni mahususi kwake kwani jicho hilo linasimama kama uangalizi kutoka kwa Mungu na pia ni jicho la utoaji.

Mjasiriamali huyo wa bidhaa za urembo pia alieleza kwamba jicho hilo kwenye utambulisho wake linamkumbusha mara kwa mara kwamba kila anachofanya binadamu kinaangaliwa na jicho la Mungu lisilolala wala kusinzia.

Aidha, Huddah Monroe alikiri kufahamu kwamba Mungu katika jumuiya ya Freemason anatambulika kama mjenzi mkuu wa Ulimwengu na vyote vilivyomo.

“Kuhusu picha yangu ya wasifu - JICHO LA UTOAJI ! JICHO LA MUNGU! Macho ya kuona yote…. 💫 Inatumika kama ukumbusho kwamba mawazo na matendo ya wanadamu daima huzingatiwa na Mungu mweza yote—ambaye anatajwa katika Masonry kama Mbuni Mkuu wa Ulimwengu……” Huddah alieleza kabla ya kufungia kipengele cha kuwezesha watu kutoa maoni yao.

Kwa muda mrefu, Huddah Monroe amekuwa akitumia picha ya rais wa kwanza na mwanzilishi wa taifa la Kenya Mzee Jomo Kenyatta.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved