logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Zari aibuka na mtindo mpya wa nywele fupi

Mama huyo wa watoto watano katika miezi ya hivi karibuni amekuwa akipunguza kuweka wazi kuhusu maisha yake ya mitandaoni.

image
na Davis Ojiambo

Burudani01 July 2024 - 10:19

Muhtasari


  • • Mama huyo wa watoto watano katika miezi ya hivi karibuni amekuwa akipunguza kuweka wazi kuhusu maisha yake ya mitandaoni.
ZARI

Mwanasosholaiti Zari Hassan ameanza mwezi mpya wa Julai kwa kuzindua mtindo mpya wa nywele fupi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zari alichapisha rundo la picha zake akionyesha muonekano wake mpya, huu akijivunia mtindo wa nywele fupi.

“Ikiwa inakufurahisha, basi sio kupoteza wakati #shorthairvibes” Zari aliandika kwenye picha hizo.

Mashabiki wake walimsifia kwa muonekano mpya, wengine wakimtaka kudumisha muonekano huo badala ya ule wa mawigi marefu.

Haya hapa ni baadhi ya maoni ya mashabiki wake;

“Je, unaweza kuweka nywele hii kama milele?   😃 Inaonekana vizuri sana kwako. Kuzeeka nyuma!!!!” Ruth Klenam.

“Ni mrembo kweli, likes za zari jman’ Martha Raphael.

“Nywele inaonekana ya kushangaza kwako.” Galston Anthony.

“Yeye ndiye mwanamke mrembo zaidi nchini Uganda na Afrika Kusini” Rodney Greyssal.

Mama huyo wa watoto watano katika miezi ya hivi karibuni amekuwa akipunguza kuweka wazi kuhusu maisha yake ya mitandaoni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved