Zuwena wa Tanzania aeleza kwa nini hawezi kuchumbiana na mwanamume Mkenya

"Siwezi kamwe kuwa na mwanamume Mkenya, jinsi walivyo . Kwa Kiswahili chao kile?" alisema.

Muhtasari

•Kulingana naye, wanaume wa Kenya hawatumii lugha ya 'kimapenzi'.

Zuwena
Image: HISANI

Video vixen wa  Tanzania Zuwena wa Diamond amesema hatawahi kuchumbiana na mwanamume Mkenya.

Kulingana naye, wanaume wa Kenya hawatumii lugha ya 'kimapenzi'.

"Siwezi kamwe kuwa na mwanamume Mkenya, jinsi walivyo . Kwa Kiswahili chao kile?"

Aliendelea kulalamika kuhusu jinsi wanamume wa Kenya wanavyomwalika mwanamke bila ya mapenzi.

'Si Ukuje'

Heri nikae na boy Wangu Philipo, mtu mweupe, mtoto white."

Katika siku za nyuma, mastaa mbalimbali wa Kenya walifichua kuwa hawatapatikana wakiwa na wanaume Wakenya.

Miongoni mwao ni Huddah Monroe na Shakila

Kulingana naye angependelea kuchumbiana na wanaume wa Nigeria, ambao aliwasifu kwa ukarimu wao.

Akiongea kwenye kipindi cha Moja kwa Moja ya Instagram, alisema

'Wanaijeria ndio watu watamu zaidi unaoweza kukutana nao, wanakupa pesa na kukutendea wema

Siwezi kuchumbiana na Mkenya kamwe. Mimi si Mkenya kwa hivyo nina haki ya kufanya hivyo. "

Je, unaweza kum'cheat mpenzi wako katika mazingira gani?

"Sitaki, kwa hivyo Mungu anisaidie."

Shakilla aliongeza kuwa kosa lake baya zaidi alilowahi kufanya ni kuwaamini watu wasio sahihi

"Kuburudisha marafiki wasiofaa, najuta kabisa na kuwa mzuri kwa watu wasiofaa. Ilinigharimu sana."

Huddah alisema kabisa wanaume wa Kenya sio wa aina yake.

Katika kurasa zake maarufu za mitandao ya kijamii, sosholaiti huyo na mfanyabiashara  wa vipodozi alidokeza kwamba watu wa nchi yake ni wabahili.

“Sichumbi na Wakenya. Sijui mara ya mwisho kuwa na Mkenya,” aliandika Huddah.

Kisha akasema, “Nawaona wanaume wote wa Kenya kama ndugu zangu.”