Justin na Hailey Bieber watangaza kuzaliwa kwa mtoto wao wa kwanza

Katika tangazo kwenye akaunti yake, Bieber aliweka picha ya mguu mdogo wa mtoto wake mvulana.

Muhtasari

•"Karibu nyumbani," Bieber aliandika katika ukurasa wake mapema Jumamosi, na kufichua jina la mtoto huyo - Jack Blues Bieber.

Image: BBC

Mwimbaji wa Canada Justin Bieber ametangaza kuzaliwa kwa mtoto wake wa kwanza na mkewe Hailey Bieber.

Katika tangazo kwenye akaunti yake ya Instagram, Bieber aliweka picha ya mguu mdogo wa mtoto wake mvulana.

"Karibu nyumbani," Bieber aliandika katika ukurasa wake mapema Jumamosi, na kufichua jina la mtoto huyo - Jack Blues Bieber.

Katy Perry na Kylie Jenner ni miongoni mwa watu mashuhuri ambao waliwapongeza wawili hao.

Justin na Hailey Bieber walifunga ndoa katika sherehe ya faragha mjini New York mwaka 2018.