Usiwekeze hisia katika ndoa na uhusiano wa maceleb, tutakuvunja moyo - Akothee aonya

"Mahusiano si ya watu wanyonge, lakini mapenzi ni matamu,” alisema

Muhtasari

•Akothee alibainisha kuwa watu mashuhuri mara nyingi hutumiwa kama mifano ilhali hata watu wa kawaida hupitia maswala sawa.

•Pia alitoa ushauri kwa Bi Lopez akimtaka kuchukua hatua yoyote anayotaka kuchukua katika siku zijazo.

Image: FACEBOOK// AKOTHEE

Mwimbaji na mjasiriamali maarufu wa Kenya Esther Akoth almaarufu Akothee amewaonya watu dhidi ya kuwekeza hisia zao katika mahusiano na ndoa za watu mashuhuri.

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 43 ambaye amewahi kuwa kwenye mahusiano kadhaa alitoa maoni hayo alipokuwa akitoa maoni  kuhusu talaka ya mwimbaji Jennifer Lopez na mwigizaji Ben Afflek.

Wakati akitoa maoni yake, Akothee alibainisha kuwa kwa kawaida watu huwa wanazungumza sana watu mashuhuri wanapopitia matatizo ya mahusiano, tofauti na watu wa kawaida wanapopitia masuala sawa.

Akothee alibainisha kuwa watu mashuhuri mara nyingi hutumiwa kama mifano ilhali hata watu wa kawaida hupitia maswala sawa.

“Kuishi na mtu mwingine kunaweza kuwa jambo gumu sana—mara nyingi watu hupambana nalo! Sikuwahi kuelewa kabisa ugumu wa maisha ya mapenzi ya Jennifer Lopez hadi nilipojikuta katika hali kama hiyo ya fujo. Ukweli ni kwamba, unapaswa tu kuchuna sumu yako, umeze, na kuendelea,” Akothee alisema kupitia Instagram

Aliongeza, "Watu mashuhuri mara nyingi ni mifano kuu ya mahusiano yasiyofanya kazi, uchumba wa mapema, na ndoa iliyoahirishwa. Sio kwamba watu wasio maarufu hawapati maswala sawa - kwa kweli, hali zao zinaweza kuwa mbaya zaidi."

Walakini, mahusiano ya mtu mashuhuri yanapovunjika, yanachukuliwa kama habari mpya, na ulimwengu unakataa kuendelea.

Mama huyo wa watoto watano aliwaomba watu waache kuzingatia sana mahusiano ya watu mashuhuri wakibainisha kuwa si mara zote huenda vizuri.

Pia alitoa ushauri kwa Bi Lopez akimtaka kuchukua hatua yoyote anayotaka kuchukua katika siku zijazo.

"Ni wakati muafaka watu kuacha kuwekeza hisia zao katika ndoa za watu mashuhuri na uhusiano. Tutaachana na kuwakatisha tamaa kila siku.🤣🤣," alisema.

“Namtakia kila la heri Jennifer. Kwake, nasema, "Mama, usiondoke au kurudi sokoni; kaa tu. Ikiwa unahisi kurudi kwa Ben, na moyo wako bado unapiga kwa ajili yake, waite wanasheria wa talaka na uwaambie waweke. pause kwa upuuzi huo kwa sasa 🤣🤣 Unaweza kuwasasisha tena baadae mambo yanapoharibika Mahusiano si ya watu wanyonge, lakini mapenzi ni matamu,” aliongeza.