logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Grace Mapunda: Muigizaji wa muda mrefu wa filamu Tanzania amefariki dunia

Mpaka kufariki kwake, Mapunda alikuwa anaigiza kama Tesa kwenye Tamthilia ya Huba kwenye Maisha Magic Bongo.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani02 November 2024 - 09:18

Muhtasari


  • Haya ni kwa mujibu wa waigizaji wenzake katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
  • Jiffy Pictures yake Lulu Hassan pia imetoa taarifa hizo ikimumboleza kama mtu aliyejitolea katikakazi yakevya uigizaji.



Muigizaji wa muda mrefu wa filamu za Kiswahili kutoka Tanzania, Grace Mapunda ameripotiwa kufariki dunia.

Haya ni kwa mujibu wa waigizaji wenzake katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

Jiffy Pictures yake Lulu Hassan pia imetoa taarifa hizo ikimumboleza kama mtu aliyejitolea katikakazi yakevya uigizaji.

Mpaka kufariki kwake, Mapunda alikuwa anaigiza kama Tesa kwenye kipindi cha Huba ambacho kinazalishwa na Jiffy Pictures ya Lulu Hassan na Rashid Abdalla kwenye Maisha Magic Bongo.

“Tumeondokewa Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu na Kwake ni marejeo,Kwaniaba ya Familia ya Grace mapunda tunawajulisha kua Mama yetu Mpendwa Grace Mapunda (TESA) hutupo nae tena Duniani,Bwana ametoa,Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe,” Jiffy Pictures walitoa sasisho kupitia ukurasa wao wa Facebook asubuhi ya Novemba 2.

Taarifa mbalimbali zinadai kwamba Mapunda alifariki hospitalini baada ya kulazwa kwa muda mfupi ambapo alilazwa Novemba 1.

Grace Mapunda atakumbukwa kwa mchango wake kwenye sekta ya maigizo, akicheza kama Mama mzazi wa mastaa wengi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved