logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diana Marua amshauri bintiye kumzalia wajukuu 5

Diana Marua ni mama kwa watoto 5, watatu wakiwa wale aliowazaa, mmoja akiwa wa kuasiliwa na mwingine akiwa ni wa mumewe na mpenzi wake wa ujanani, Yvette Obura.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani19 November 2024 - 13:14

Muhtasari


  • Binti huyo alisema kwamba angependa kuzaa watoto 5 lakini akasema kwamba atafurahi zaidi iwapo atapata 2 tu.
  • Mtoto huyo alisema kwamba anachagua 2 kwa sababu watamrahisishia kazi ya malezi, jambo ambalo mamake alimtaka kufikisha 5 akimpa hakikisho la kumsaidia katika malezi.



RAPA na mtengeneza maudhui, Diana Marua amemshauri binti yake mzaliwa wa kwanza, Heaven Bahati umuhimu wa kuzaa watoto angalau 5.

Akizungumza naye wakati walikuwa kwenye ziara ya mama na binti ndani ya gari lao, Diana Marua alilenga kujua maazimio ya binti yake kuhusu familia katika maisha yake ya baadae.

Binti huyo alisema kwamba angependa kuzaa watoto 5 lakini akasema kwamba atafurahi zaidi iwapo atapata 2 tu.

Mtoto huyo alisema kwamba anachagua 2 kwa sababu watamrahisishia kazi ya malezi, jambo ambalo mamake alimtaka kufikisha 5 akimpa hakikisho la kumsaidia katika malezi.

“Mimi nataka kupata watoto 5 kama wewe,” Heaven Bahati alimwambia mamake mwanzoni.

“Nikikua mtu mzima ningependa lakini kuwa na watoto 2 tu. Kwa sababu sitaki kulea watoto wengi. Kulea watoto wengi ni kazi ngumu,” mtoto huyo alibadili msimamo wake baada ya mamake kumuuliza sababu ya kutaka watoto.

Baada ya kusisitiza, akiambatanisha na sababu za kutaka watoto 2 pekee, Diana Marua alimshauri bintiye kwa kumbembeleza kupata watoto 5 angalau.

Marua alimwambia bintiye kwamba kupata watoto 5 ni vizuri, akimhakikishia kwamba atakuwa tayari muda wote kumpa msaada wa malezi.

“Hivyo unasema unataka watoto 2? Hapana, ningependa upate watoto 5 kama ulivyosema awali. Najua ni shinikizo kubwa kulea watoto 5 lakini ningependa kukuhakikishia kwamba wakati utakuwa unahisi ni mzigo mzito, wewe walete tu kwangu. Mimi nitakuwa nyanya yao na nitawalea,” Diana Marua alimshauri bintiye.

Mwisho wa siku, binti huyo alishawishika na ushauri wa mamake kuhusu kupata watoto 5 lakini kwa sharti moja.

“Ndio nitapata watoto 5 lakini kama hawatakuwa wasumbufu. Kama hawatakuwa wananiita ita kila mara wakiniomba hiki na kile. Mwingine anasema sitaki kipakatalishi, nataka simu,” Heaven Bahati alisema.

Diana alimwambia kuwa hivyo anavyosema hataki kuja kusumbuliwa na wanawe ndivyo wanavyomsumbua, shtaka ambalo bintiye alijitetea kwamba yeye si msumbufu vile.

Diana hata hivyo alimhakikishia kwamba hawamsumbui bali ni furaha yake kuona uzao wat umbo lake wakimuitisha hiki na kile.

Diana Marua ni mama kwa watoto 5, watatu wakiwa wale aliowazaa, mmoja akiwa wa kuasiliwa na mwingine akiwa ni wa mumewe na mpenzi wake wa ujanani, Yvette Obura.


 


 


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved