logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mr P amsherehekea pacha wake, Rudeboy siku yao ya kuzaliwa licha ya kuwepo kwa ugomvi baina yao

Hii ni licha ya Rudeboy kumburuza hadi kwa kutumia wakili akidai kwamba pcha wake aliiba wimbo wake na kuutoa bila ridhaa yake.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani20 November 2024 - 09:46

Muhtasari


  • Awali, Radiojambo.co.ke iliripoti kuwa Paul Okoye, almaarufu Rude Boy, alimshutumu Bw P na mtayarishaji wao wa zamani, Vampire, kwa kuiba nyimbo zake.
  • Alifichua kuwa alikuwa ameandika na kurekodi wimbo unaoitwa ‘Winning,’ ulionuiwa kuwa sehemu ya albamu yake ijayo mwaka ujao.
  •  Hata hivyo, alidai kwa mshangao kwamba Mr. P alitoa wimbo huo kupitia kwa mtayarishaji huyo.



Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo kutoka Nigeria Peter Okoye, maarufu kama Mr P ameonyesha ukomavu wake kiakili kwa kuweka uadui na ugomvi wake na kakake kando wakati anasherehekea siku yao ya kuzaliwa.

Mr P alichukua kwenye kurasa zake kwenye mitandao ya kijamii na kuchapisha picha zao za utotoni na wakiwa watu wazima na kufuatisha na ujumbe wa kusherehekea siku ya kuzaliwa na pacha wake, Paul Okoye maarufu kama Rudeboy.

Hii ni licha ya Rudeboy kumburuza hadi kwa kutumia wakili akidai kwamba pcha wake aliiba wimbo wake na kuutoa bila ridhaa yake.

Awali, Radiojambo.co.ke iliripoti kuwa Paul Okoye, almaarufu Rude Boy, alimshutumu Bw P na mtayarishaji wao wa zamani, Vampire, kwa kuiba nyimbo zake.

Alifichua kuwa alikuwa ameandika na kurekodi wimbo unaoitwa ‘Winning,’ ulionuiwa kuwa sehemu ya albamu yake ijayo mwaka ujao.

Hata hivyo, alidai kwa mshangao kwamba Mr. P alitoa wimbo huo kupitia kwa mtayarishaji huyo.

Akijibu madai hayo, Mr. P alieleza kuwa wimbo huo aliutunga yeye na Calypso60. Alidai kuwa haiwezekani kwake kuiba wimbo alioshirikiana nao, kama alivyodai pacha wake.

Licha ya madai hayo yanayoendelea, Peter bado alikiri na kumsherehekea kaka yake katika siku yao maalum. Alitumia ukurasa wake wa Instagram kushiriki picha zao nzuri za kujirusha.

Aliandika picha hizo, “HAPPY BIRTHDAY TO US! Endelea KUSHINDA! 🎂🎂🎂🙅🏽🙅🏽🎂🎂🎂#WinningSeaon +1.”

Mapacha hao wawili kutoka kwa bendi iliyosambaratika ya PSquare wamekuwa katika hali ya mfarakano kwa miezi kadhaa sasa.

Ugomvi wao ulianza mnamo mwaka 2015 lakini baada ya miaka kadhaa walitangaza kusameheana na kurudiana mwaka 2021

Baada ya uvumi wa kuachana, wawili hao walionyesha hadharani ufa mkubwa katika undugu wao mwaka 2017 walipofarakana hadharani kupelekea kusitisha shoo zao walizokuwa wameziratibu kufanyika Marekani na Kanada wakati huo.

Baada ya kurekebisha uhusiano wao 2021, waliingia studio na kuachia wimbo kwa jina ‘Jaiye’ ambao hata hivyo ulifanikiwa kuwaweka pamoja kwa kipindi kifupi.

Walikorofishana tena mwaka jana ambapo wamekuwa wakituhumiana kwa sakata mbalimbali ambazo ziliangusha PSquare.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved