logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Will Smith ajitenga na madai ya kuhusishwa na sherehe za P-Diddy

Msaani Will Smith amefunguka kuhusu tuhuma ya kujihusisha katika sherehe ya 'Freak Off Party'

image
na OTIENO TONNY

Burudani16 December 2024 - 11:34

Muhtasari


  • Nyota huyo wa filamu ambaye alizaliwa Septemba 1998 alikanusha uvumi huo akidai kwamba kwamba hauna msingi

caption

Willard Carroll Smith II maarufu kama Will Smith amekana madai yanayomhusisha na msaani wa rap P-Diddy ambaye alikamatwa na kushtakiwa kwa tuhuma  ya kujihusisha katika ulanguzi wa binadamu na hatia nyinginezo.

Mwanafilamu na  mwimbaji huyo  wa nyimbo za rap maarufu kama Will Smith mwishowe alifunguka na kuzungumza kuhusu tuhuma kuwa alijihusisha katika sherehe za rafiki yake P-Diddy, sherehe iliyobahatizwa kama Freak off Party ambapo inadaiwa kuwa hatia kadhaa za kingono zilifanyika.

Nyota huyo wa filamu ambaye alizaliwa 25 Septemba 1998 alikanusha uvumi huo kuwa hauna msingi. Akiongea katika tamasha moja eneo la Sandiego, Califonia, Smith alisema kuwa uvumi huo ni mbaya na unafaa kukoma.

‘’Nimekuwa nikiona utani na kila kitu, nyingine zinafurahisha na nyingine zinahuzunisha. Nataka  kuweka hili wazi kabisa: Sina chochote cha kufanya na Puffy, kwa hivyo unaweza kuacha huo utani . Na mkome huo upuuzi. Sijafika popote karibu na "Freak Off." Alisema Smith.

Nyota huyo wa kuigiza aliendelea kukanusha  kuwa hajawaifanya hayo mambo aliyoyaita ya kijinga wala hapendi mafuta ya watoto. Maoni haya yanakuja baada ya chupa kadhaa za mafuta za watoto kupatikana katika mojawapo ya makao ya P-Diddy wakati maafisawauchunguzi wa biashara ya ngono kuvamia jumba lake.

Smith alimaliza kwa kusema kuwa anafanya vitu vyake kibinafsi na hahitaji kuhusishwa na vitu vya watu wengine.

P-Diddy bado yuko korokoroni anakozuiliwa Brooklyn, New York huku akichunguzwa kwa madai ya kesi kadhaa ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia, biashara ya ngono, ulaghai na kuwezesha ukahaba.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved