logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Nimepata Wafuasi Wapya 100k TikTok Na 150k YouTube” – Willy Paul

“Wakenya Wamefanya. Tik Tok Yangu Imepata Wafuasi 100k Zaidi, YouTube Yangu Imevutia Wafuatiliaji 150k Zaidi,” Willy Paul alifichua.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani17 December 2024 - 10:12

Muhtasari


  • Msanii huyo zamani akiwa wa injili hakusita kutambua kwamba hizo kwa asilimia kubwa ni juudi za mashabiki wake wa Kenya.
  • “Wakenya Wamefanya. Tik Tok Yangu Imepata Wafuasi 100k Zaidi, YouTube Yangu Imevutia Wafuatiliaji 150k Zaidi,” Willy Paul alifichua.



MSANII wa kizazi kipya nchini Kenya, Willy Paul amefichua kwamba kipindi cha wiki moja iliyopita kimekuwa kipindi cha mavuno makubwa kwa upande wake.


Pozee ambaye amekuwa midomoni mwa watu wengi tangu usiku wa Desemba 7 wakati wa mfarakano ulioshuhudiwa katika tamasha la Furaha Fest jijini Nairobi, amefichua kwamba akaunti zake za mitandao ya kijamii zimeshiba pakubwa kwa kipindi hicho.


Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Willy Paul alifichua kwamba amepata wafuasi wapya zaidi ya laki moja kwenye TikTok na wengine wapya zaidi ya laki na nusu kwenye chaneli ya YouTube.


Msanii huyo zamani akiwa wa injili hakusita kutambua kwamba hizo kwa asilimia kubwa ni juudi za mashabiki wake wa Kenya.


“Wakenya Wamefanya. Tik Tok Yangu Imepata Wafuasi 100k Zaidi, YouTube Yangu Imevutia Wafuatiliaji 150k Zaidi,” Willy Paul alifichua.


Willy Paul baada ya kufarakana na usimamizi wa Diamond Platnumz katika tamasha la Furaha Fest lililoandaliwa katika Polo Club, amekuwa katika mstari wa mbele kudai kwamba ndiye mpiganaji mkuu wa haki sawa kati ya wasanii wa Kenya na wasanii wa kigeni.


Msanii huyo alidaiwa kuzushiana vurugu baada ya ratiba ya kutumbuiza kwake kubadilishwa kinyemela, vurugu ambazo zilimfanya Diamond kutopata nafasi ya kutumbuiza katika usiku huo wa tafrija.


Hata hivyo, baadae katika taarifa yake kwa njia ya video, Diamond alikanusha kwamba kutotumbuiza kwake hakukuwa na uhusiano wowote na Willy Paul bali ni wasimamizi walifeli katika kuhakikisha kuna utulivu.


Msanii huyo wa Bongo alifichua kwamba alilipwa zaidi ya shilingi milioni 19 za Kenya na kudokeza kwamba asingerudisha hata senti baada ya kutotumbuiza, kwani waandalizi ndio walienda kinyume na maagano ya mkataba wa ujio wake.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved