logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Filamu kwa jina ‘’Making of a Bad Boy’’ kuhusu P-Diddy kupeperushwa Januari 14

Matarajio yako juu kuhusu filamu ya Peacock kwa jina ''Diddy: The Making of a Bad Boy'' ambayo ni hadithi ya dakika 90 kuhusu maovu ya P-Diddy.

image
na OTIENO TONNY

Burudani08 January 2025 - 12:08

Muhtasari


  • Mwimbaji na mtayarishaji wa nyimbo na filamu Al B, atazungumza kwa mara ya kwanza kuhusu uhusiano wake na Kim Porter kabla hajachumbiana na Combs.
  • Itakumbukwa kuwa Combs pia amekabiliwa na mashtaka zaidi ya 25 ya madai yake ya utovu wa maadili ya ngono miongoni mwa madai mengine.



Filamu ambayo inatarajiwa kuweka wazi baadhi ya madhambi ambayo msaani na mwanafilamu tajika P-diddy aliyafanya sasa inasubiriwa kwa hamu na ghamu ikitarajiwa kuonyeshwa kwa mara ya kwanza kupitia Peacock.

Kionjo cha ‘’The Making of a Bad Boy’’ imefichua kuwa watu wa karibu wa Combs, akiwemo mlinzi wake wa zamani, mfanyakazi wa ndani, msanii wa kupodoa na mtayarishaji ni miongoni mwa wanaohojiwa kwenye filamu hiyo.

Mwimbaji na mtayarishaji wa nyimbo na filamu Al B, atazungumza kwa mara ya kwanza kuhusu uhusiano wake na Kim Porter kabla hajachumbiana na Combs

Itakumbukwa kuwa Combs pia amekabiliwa na mashtaka zaidi ya 25 ya madai yake ya utovu wa maadili ya ngono miongoni mwa madai mengine.

Msaani huyo mwenye umri wa miaka 55 anazuiliwa  katika gereza la Metropolitan Detention Center huko Brooklyn, New York, tangu Septemba, alipokamatwa kwa makosa ya biashara ya ngono na ulaghai. Majaji watatu tofauti wamemnyima dhamana kwa nyakati tatu tofauti.

Mawakili wa Sean "Diddy" Combs hata hivyo walikosoa filamu hiyo katika taarifa waliotoa kupitia  jarida la Newsweek siku ya Ijumaa.

"Filamu hizi ni pamoja na madai ambayo hayajadhibitiwa na hutoa majukwaa ya nadharia za njama zisizo na msingi bila uwajibikaji au ushahidi. Kwa upande wa filamu ya Peacock haswa, motisha na uaminifu wa wale wanaohojiwa lazima utiliwe shaka. Wengi hudai kuwa na ujuzi lakini hawana uhusiano wowote na ukweli, huku nadharia zao potovu, zisizo na msingi zikikatwa na kusisitizwa ili zionekane kuwa za kweli,’’ Hii ni mujibu ya mawakili hao kupitia jarida la Newsweek.

Kesi ya biashara ya ngono ya Combs inatarajiwa kuanza mjini New York Mei 5 mwaka huu wa 2025.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved