logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Charlene Ruto Atangaza Shindano Jipya Kwa Vijana Kujishindia Hadi Sh195,000

Kupitia ukurasa wake wa X, binti wa kwanza wa rais Ruto alifichua kwamba vijana wenye talanta katika ubunifu wa mitandaoni wenye kati ya umri wa miaka 18 hadi 35 wanaweza jiandikisha.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani11 January 2025 - 12:00

Muhtasari




    BINTI wa rais, Charlene Ruto ametangaza ujio wa shindano lake jipya kwa vijana ambalo litafanyika mwezi ujao.


    Kupitia ukurasa wake wa X, binti wa kwanza wa rais Ruto alifichua kwamba vijana wenye talanta katika ubunifu wa mitandaoni wenye kati ya umri wa miaka 18 hadi 35 wanaweza jiandikisha.


    Alisema kwamba ili kujisajili, vijana ni sharti wajiunge kwa makundi ya watu 3 na kuonyesha ueledi wao katika suala la kubuni wavuni, kujisajili kutaendelea hadi Februari 11.


    “Ni wakati wa jambo letu kubwa linalofuata…. Mashindano ya Tovuti! Je, wewe ni kati ya miaka 18-35? Ungana katika vikundi vya watu 3 na utuonyeshe ulichonacho! Changamoto itafunguliwa: 11 Januari 2025. Makataa ya kuwasilisha: 11 Februari 2025, saa sita usiku. Hatua za kuhitimu:


    1 Shiriki viungo vya tovuti 3 bora ambazo timu yako au wanachama wameunda.


    2️ Tutumie pendekezo fupi la kiufundi la tovuti ambayo ungeunda kwa ajili ya TYPNI.


    3️ Ambatisha vitambulisho na wasifu wa washiriki wote 3 wa timu.


    Shinda $1,500 USD! Wacha tuone ubunifu wako unang'aa. Tayari? Hebu tufanye hivi!” Charlene aliandika.


    Hii si mara ya kwanza kwa binti wa rais kutangaza shindano la kuwakimu vijana wenye ujuzi katika ubunifu wa mtandaoni.


    Mwaka jana, binti Ruto alitangaza shindano sawia na hilo lililofanyika majira sawia, na tuzo kwa mshindi ilikuwa shilingi laki moja taslimu.


    Kando na taslimu, Charlene Ruto wakati huo alitangaza kula chakula cha mchana na mshindi katika mgahawa wa kifahari.


    “Mtandao wa Vijana wa Kimataifa (TYPNI) unatafuta nembo bainifu inayojumuisha ari ya ujana na ubunifu. Shindano hili linatoa fursa kwa wabunifu wachanga kuonyesha vipaji vyao na kuchangia utambulisho mahiri wa TYPNI,” aliandika kwenye bango hilo kwenye mtandao wa X.



    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved