logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Mtasema Na Mtalala!” Rachel Awazima Wanaomkosanisha Na Familia Ya Otuoma

“Mama mimi nakupenda sana, na vile huyu mtoto wako alikuwa anakupenda, hivyo hivyo ndivyo na mimi nitazidi kukupenda.” Rachael alimwambia mama mkwe wake.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani12 January 2025 - 14:35

Muhtasari


    RACHAEL Otuoma amevunja kimya kuhusu uvumi unaoenezwa kwamba huenda kuna matatizo ya kutoelewana baina yake na familia ya marehemu mume wake, Ezekiel Otuoma.


    Akizungumza wakati wa mazishi ya Ezekiel Otuoma Jumamosi katika kaunti ya Siaya, mrembo huyo alisema kwamba watu hawakosi la kusema lakini kwake hawatoboi.


    Rachael alionyesha kwamba kuna uhusiano mzuri tu baina yake na familia ya marehemu mumewe, haswa mama mkwe, mwanamke ambaye alimtaja kama nguzo muhimu katika maisha yake.


    Rachael alisema kwamba watu watasema huko nje na mwisho wa siku watalala, kwani yao wenyewe ndio wanayajua hata kama watu wa nje wanajaribu kuingilia.


    “Kwa mama mkwe, huyu mwanamke ananipenda sana bwana. Mtasema hapo nje lakini mtalala. Za watu kwa nyumba zao mtajaribu kunyoosha vidole lakini sisi wenyewe ndio tunajuana,” Rachael alisema.


    Aliahidi kutumia heshima na taadhima ya marehemu mumewe kueneza upendo wake kwa mama mkwe.


    “Mama mimi nakupenda sana, na vile huyu mtoto wako alikuwa anakupenda, hivyo hivyo ndivyo na mimi nitazidi kukupenda. Nitampa Otuoma heshima yake vile alikupa heshima yako na vile alinipa heshima yangu,” Rachael alimwambia mama mkwe wake.


    Kabla ya Otuoma kufa, kulikuwa na sekeseke kwamba mrembo huyo alikuwa na mtafaruku na wakwe zake, jambo ambalo lilikuwa linazua mjaala mkali kwenye TikTok mara kwa mara.


    Hata hivyo, Rachael amesisitiza kwamba ni Amani tu kwenda mbele baina yake na wakwe zake, hata akiahidi kwamba atadumisha upendo huo si tu kwa mama mkwe lakini pia kwa binti wa Otuoma ambaye alizaa na mwanamke mwingine.


    Mwanasoka huyo alizikwa Jumamosi nyumbani kwao katika kaunti ya Siaya, takribani wiki tatu tangu alipofariki.


    Otuoma alifariki siku chache kuelekea Krismasi mwaka jana baada ya miaka 4 ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa Motor Neurone – ugonjwa ambao wataalamu wa afya ya mwili wanauelezea kama tatizo la kufifisha neva za mwili.


    Alipatikana na ugonjwa huo mwaka 2020 na mkewe Rachael amekuwa upande wake kwa kipindi chote haki kifo chake, na alifichua kwamba huu ulikuwa mwaka wa kuadhimisha miaka 10 ya ndoa yao.



    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved